Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 2:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Nitafanya agano na nyama wa pori, ndege pamoja na vyote vinavyotambaa, kusudi wasikuumize. Nitaondoa upinde, upanga na silaha za vita katika inchi, na kukufanya uishi kwa usalama.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 2:20
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na viumbe vyote vyenye uzima, ndege, nyama wa kufugwa na wa pori, wote waliotoka katika chombo pamoja nanyi.


Mungu atafanya hukumu kati ya mataifa; ataamua maneno kati ya watu wengi. Watu watafua panga za vita kuwa majembe na mikuki yao kuwa visu vya kuvuna. Taifa halitapigana na taifa lingine wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.


Hautaitwa tena: Aliyeachwa, wala inchi yako haitaitwa: “Ukiwa”. Lakini utaitwa: “Ninamufurahia”, na inchi yako itaitwa: “Aliyeolewa”. Maana Yawe amependezwa nawe, naye atakuwa kama mume wa inchi yako.


Nitawapa moyo wa kujua kwamba mimi ndimi Yawe. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; maana watanirudilia kwa moyo wao wote.


Usiogope ee Yakobo, mutumishi wangu, wala usifazaike, ee Israeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Maana nitakuokoa toka huko mbali unapokuwa, nitawaokoa wazao wako kutoka katika uhamisho. Utarudi na kuishi kwa amani, wala hakuna mutu atakayekuogopesha.


Nitafurahi kuwatendea mema; nitawasimika siku zote katika inchi hii na kuwatendea kwa uaminifu.


Siku zinakuja ambapo nitawaazibu wote waliotahiriwa kimwili tu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Ni kusema nitawaazibu:


Mimi nitafanya agano nawe, nawe utatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nilipopita tena karibu nawe, nikakuona. Wakati huu, ulikuwa umefikia umri wa kupendwa kama binti. Nikalitandaza vazi langu juu yako na kuufunika uchi wako. Nikafanya nawe agano la ndoa, nawe ukakuwa wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Nitafanya nao agano la amani. Nitaondoa nyama wakali katika inchi, kusudi kondoo wangu wakae katika mbuga kwa usalama na kulala katika pori.


Miti inayokuwa katika mashamba itazaa matunda, udongo utatoa mazao kwa wingi, nao wataishi kwa salama katika inchi yao. Nitakapovunja nira zao za utumwa na kuwaokoa toka katika mikono ya hao waliowafanya kuwa watumwa halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Ndivyo nitakavyofanya kusudi yote yaone ukubwa wangu na utakatifu wangu. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Yawe anasema: Lakini mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri; hakuna mungu mwingine lakini mimi, wala hakuna anayeweza kuwaokoa.


Maana, nitalifanya jina la Bali lisitajike tena katika kinywa chako.


Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka, kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.


Kupepeta ngano kutaendelea mpaka wakati wa kuvuna zabibu, na mavuno ya zabibu mpaka wakati wa kupanda mbegu. Mutakuwa na chakula tele na kuishi kwa usalama katika inchi yenu.


Nitawapa amani katika inchi hata muweze kulala bila kuogopeshwa na chochote. Nitaondoa nyama wakali katika inchi na inchi yenu haitapatwa na vita.


Mungu atatoa hukumu kati ya mataifa mengi, atakata mashauri ya mataifa makubwa ya mbali. Nayo yatafua mapanga yao kuwa majembe, na mikuki yao kuwa visu vya kuvuna. Taifa halitapigana na taifa lingine, wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.


Ataondoa kabisa magari ya vita katika inchi ya Efuraimu, na farasi wa vita kutoka katika Yerusalema; pinde za vita zitatupwa mbali. Naye ataleta amani kati ya mataifa; utawala wake utaenea toka bahari mpaka bahari, toka muto Furati hata miisho ya dunia.


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


“Baba yangu, umeweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana na yeyote ambaye Mwana anataka kumujulisha kwake.”


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


Ninyi hamumujui, lakini mimi ninamujua. Kama ningesema kwamba simujui, ningekuwa mwongo kama ninyi. Lakini ninamujua na ninashika neno lake.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Bila shaka, ninahesabu mambo yote kuwa kihombo kwa ajili ya faida kubwa ya kujua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimekubali kupoteza vyote, nikivihesabu kuwa kama mavi, kusudi nimupate Kristo


Hivi, mutaweza kuishi sawa Bwana anavyotaka na kumupendeza katika mambo yote. Kwa njia hiyo mutafikia kufanya matendo mema ya kila namna na kuzidi kumujua Mungu.


na kwa sababu hiyo ninapata mateso haya. Lakini sisikii haya kwa ajili ya ile. Maana ninajua ni nani yule niliyemwamini, nami ninahakikisha kwamba anaweza kuchunga kile alichonipa kwa kunilinda mpaka Siku ile ya kurudi kwake.


Hakutakuwa tena atakayefundisha mwanainchi mwenzake, au kumwambia ndugu yake: ‘Umujue Bwana.’ Kwa maana watu wote watanijua, tangu mudogo mpaka mukubwa.


Lakini sisi ni watu wa Mungu. Mutu anayemujua Mungu anatusikiliza; yule asiyemujua Mungu hatusikilizi. Basi ni kwa njia hii tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho ya udanganyifu.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ