Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 2:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Huko nitamurudishia mashamba yake ya mizabibu. Bonde la Akori litakuwa mulango wa tumaini. Ataniitikia vizuri kama vile alipokuwa kijana, kama wakati alipotoka katika inchi ya Misri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 2:17
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wanaoabudu miungu mingine, watapata mateso mengi. Sitaitolea sadaka za damu hata kidogo, na majina ya miungu hiyo sitayataja.


Kisha, Musa pamoja na Waisraeli wakamwimbia Yawe wimbo huu: “Nitamwimbia Yawe, maana ameshinda kwa utukufu; farasi na mupanda-farasi wake amewatupa katika bahari.


Ushike mambo yote niliyokuambia. Usiyataje hata kidogo majina ya miungu mingine, hayo yasisikilike katika kinywa chako.


Basi, utawaambia hivi: Miungu hiyo ambayo haikuumba mbingu na dunia itaangamia. Itatoweka kabisa toka katika dunia, hapa chini ya mbingu.


Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.


Wakati ule, nitaondoa majina ya sanamu za miungu katika inchi, wala hayatakumbukwa tena. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondoa kabisa pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu.


Musishirikiane na mataifa haya yaliyobaki kati yenu. Musiitaje miungu yao wala musiape kwa majina ya miungu yao; musiitumikie wala kuinama mbele yao.


Halafu wakalundika mawe mengi juu yake, ambayo yako mpaka leo. Hapo hasira ya Yawe ikapoa; na pahali pale pakaitwa Bonde la Akori, ni kusema Bonde la Taabu, mpaka hivi leo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ