Unipeleke, tuende haraka, mufalme amenileta katika chumba chake. Tutafurahi na kukushangilia pamoja, tutasifu mapenzi yako kuliko divai. Wabinti wana haki ya kukupenda!
Na sasa nitawaambia jinsi nitakavyolifanya hilo shamba langu. Nitaubomoa upango wake, nalo litaharibiwa. Nitaubomoa ukuta wake, nalo litakanyagwakanyagwa.
Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.
Sanamu zake zote zitavunjwavunjwa, kila kitu kilichochumwa kitateketezwa kwa moto. Nitaharibu sanamu za miungu yake yote. Zililundikwa kutokana na mushahara wa ukahaba, nazo zitatumiwa tena kuwa mushahara wa ukahaba.
Enyi watu wa Sayuni, mulie na kugaagaa kama mwanamuke anayezaa! Maana sasa mutaondoka katika muji huu muende kukaa katika mbuga, mutakwenda mpaka Babeli. Lakini kule, mutaokolewa. Kule Yawe atawakomboa toka katika makucha ya waadui zenu.
Lakini yule mwanamuke akapewa mabawa mawili yanayokuwa kama ya tai, kusudi apate kuruka kwenda katika jangwa kwenye nafasi aliyotengenezewa, mbali na yule nyoka. Na kule apate kukulishwa kwa muda wa miaka mitatu na nusu.
Na yule mwanamuke akakimbilia katika jangwa kwenye nafasi Mungu aliyomutayarishia kusudi apate kulishwa kule kwa muda wa siku elfu moja mia mbili makumi sita.
Siku moja, mume wake akakwenda kumutafuta. Alikusudia kuongea naye vizuri na kumurudisha kwa nyumba yake. Akakwenda pamoja na mutumishi wake na punda wawili. Basi yule mwanamuke akamupeleka ndani kwa baba yake, naye baba mukwe alipomwona akamupokea kwa furaha.