Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 14:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 14:9
46 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sizani kama utafanya hivyo, kuwaua watu wa haki pamoja na waovu, kutendea watu wa haki sawa na waovu. Hapana, haiwezekani! Mwamuzi wa dunia yote hataacha kutenda mambo yanayokuwa sawa!”


Hata hivyo, mutu wa haki anashika njia yake, mutu ambaye hajafanya ubaya kwa mukono wake anazidi kuwa na nguvu.


Wenye hekima wafikiri juu ya mambo haya, watambue wema wa Yawe.


Kwa hiyo, ninafuata kanuni zako zote; ninachukia kila njia ya upotovu.


Ninajua kwamba maamuzi yako ni ya haki, ee Yawe, na kwamba umeniazibu maana wewe ni mwaminifu.


Heri wale wanaokaa ndani ya nyumba yako, wakiimba sifa zako siku zote.


Wanapopita katika bonde lenye kukauka la Baka, wanalifanya kuwa chemichemi, nazo mvua za kwanza zinalijaza maji.


Yawe ni kimbilio la watu wenye mwenendo sawa, lakini ataangamiza watenda maovu.


Mwenye hekima ndani ya moyo anaitwa mwenye akili; neno la kupendeza linawavuta watu.


Njia ya wenye haki ni kama mwangaza wa asubui mapema, ambao unaangaza zaidi na zaidi hata muchana kamili.


Lakini waasi na wenye zambi wote wataangamizwa pamoja; wanaomwacha Yawe watateketezwa.


Hawataelekea tena mazabahu ambazo ni kazi za vidole vyao wenyewe, wala kuzitazamia tena kazi za mikono yao wenyewe, ni kusema sanamu za mungu Ashera na mazabahu za kufukizia ubani.


Njia ya watu wa haki ni yenye kunyooka; ewe Mungu mwenye haki, unasawanisha njia yao.


Kwa hiyo mutakapokuja kunililia na kuniomba, nitawasikiliza.


Yawe akajibu na kusema hivi: Ni kwa sababu wamekataa kushika sheria yangu niliyowapa, wamekataa kutii sauti yangu na kufuata mapenzi yangu.


Nanyi mutakaporudi katika inchi yenu nitaondoa vitu vyote vichafu na machukizo yote.


Lakini ninyi munasema: Matendo ya Yawe si sawa! Musikilize sasa, enyi Waisraeli: Ninachofanya mimi si sawa? Munachofanya ninyi ndicho kisichokuwa sawa.


Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


Watu wengi wataondolewa uchafu, watatakaswa na kusafishwa. Lakini watu waovu wataendelea kutenda uovu. Hakuna hata mumoja wa hao waovu atakayeelewa; wenye hekima ndio watakaoelewa.


Lakini Yawe anayekuwa katika muji ule ni mwenye haki, yeye hatendi jambo lolote baya. Kila siku asubui anatangaza hukumu yake, kila kunapopambazuka anaitimiza. Lakini waovu hawana haya hata kidogo.


Nitawaimarisha watu wa Yuda; nitawaokoa wazao wa Yosefu. Nitawarudisha kwao kwa maana ninawaonea huruma, nao watakuwa kama vile sikuwa nimewakataa. Mimi ni Yawe, Mungu wao, nami nitayasikiliza maombi yao.


Mwana wa Mutu alikuja, yeye anakula na kunywa, nao wanasema: ‘Angalia huyu mulafi na mulevi, rafiki wa walipishaji wa kodi na watenda maovu wenzao.’ Lakini hekima ya Mungu ilionyeshwa kuwa ya haki kwa njia ya matendo yake.”


Simeoni akawabariki na kumwambia Maria, mama yake: “Mutoto huyu amezaliwa kwa sababu ya kuwaangusha na kuwasimamisha watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa kitambulisho kutoka kwa Mungu watu watakachokipinga,


Heri mutu yule ambaye sitakuwa kikwazo kwake.”


Kama nisingetenda kati yao matendo yasiyofanywa na mutu mwingine, wasingekuwa na zambi. Lakini sasa wameyaona lakini hata hivi wananichukia mimi pamoja na Baba yangu.


Halafu Pilato akamwuliza: “Ni kusema wewe ni mufalme?” Yesu akamujibu: “Wewe umesema kwamba mimi ni mufalme. Mimi nimezaliwa na kuja katika dunia kusudi nishuhudie ukweli. Wote wanaokuwa upande wa ukweli, wananisikiliza mimi.”


Anayekuwa mutu wa Mungu anasikia maneno ya Mungu. Hamusikii, kwa sababu ninyi si watu wa Mungu.”


Kisha Yesu akasema: “Nimekuja katika dunia kusudi hukumu ipate kufanyika; maana yake vipofu wapate kuona, nao wanaoona wapate kuwa vipofu.”


na kusema: “Wewe mutoto wa Shetani unayejaa udanganyifu na ukorofi wa kila namna! Wewe usiyependa kuona jambo la haki! Wewe hauchoki na kugeuza maneno ya ukweli ya Bwana!


Basi Sheria yenyewe ni takatifu na amri ni takatifu, ya haki na nzuri.


Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.


Waliimba wimbo wa Musa, mutumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana- Kondoo wakisema: “Ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makubwa na ya ajabu! Ewe Mufalme wa mataifa, kazi zako ni za haki na za kweli!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ