Basi, Yakobo akamukaribia baba yake na kumubusu, na baba yake aliposikia harufu ya nguo zake, akamubariki akisema: “Hii ni harufu nzuri ya mwana wangu. Ni kama harufu ya shamba Yawe alilobariki!
Litachanua maua kwa wingi kama waridi, litashangilia na kuimba kwa furaha. Mungu atalijalia utukufu wa milima ya Lebanoni, uzuri wa mulima Karmeli na wa bonde la Saroni. Watu watauona utukufu wa Yawe, watauona ukubwa wa Mungu wetu.
Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.
Wakati fulani, mimi nilisema kwamba wao ni muzeituni wenye majani mabichi, muzeituni muzuri na wenye matunda mema; lakini sasa, kwa ngurumo ya zoruba kubwa, nitauchoma kwa moto na kuyateketeza matawi yake.
Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.
Kweli nina vitu vyote vya lazima na zaidi kupita. Sasa kwa kuwa Epafrodito ameniletea zawadi zenu zote, ninatosheka. Zawadi hizi ni kama sadaka ya ubani yenye harufu nzuri, na kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto inayokubaliwa na Mungu na kumupendeza.