Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 14:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Yawe anasema: Nitaponyesha ukosefu wao wa uaminifu; nitawapenda tena kwa moyo wangu wote, maana sitawakasirikia tena.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 14:5
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

yeye ni kama mwangaza wa asubui, jua linapochomoza asubui isiyokuwa na mawingu. Yeye ni kama mvua inayootesha majani juu ya udongo.


Wale watakaobaki katika ukoo wa Yuda wataongezeka na kuwa wengi kama vile muti unavyotoa mizizi yake katika udongo na kuzaa matunda juu.


Mimi ni kama vile muti uliotandaza mizizi ndani ya maji; umande wa usiku unanyesha juu ya matawi yangu.


Ni kama umande wa mulima Hermoni, unaoanguka juu ya vilima vya Sayuni! Kutoka huko Yawe anatoa baraka, ndio uzima wa milele.


Inchi itoe mazao kwa wingi, vilima vijae mavuno kama ya Lebanoni, na watu wa miji wastawi kama majani.


Akuwe kama manyunyu yanayolowanisha mashamba, kama mvua inayonyeshea udongo.


Uliongoa muzabibu kutoka Misri; ukawafukuza watu wa mataifa, na kuupandikiza katika inchi yao.


Kwa macho yangu, nimeona waadui zangu wameshindwa; kwa masikio yangu, nimesikia kilio cha wanaotenda maovu.


Watu wa haki wanastawi kama mingazi; wanakomaa kama mierezi ya Lebanoni!


Kasirani ya mufalme ni kama ngurumo ya simba, lakini upendo wake ni kama umande juu ya majani.


Mupenzi wangu ni wangu, nami ni wake. Yeye anakulisha kondoo wake penye yungiyungi.


Maziba yako ni kama paa mapacha, ambao wanachungwa penye yungiyungi.


Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji.


Maana, Yawe ameniambia hivi: Tokea juu kwenye makao yangu nitaangalia yanayotukia, nikitulia kama joto katika mwangaza wa jua, kama wingu la umande wakati wa mavuno.


Wafu wako wataishi tena, miili yao itafufuka. Wanaolala katika mavumbi wataamuka na kuimba kwa furaha! Mungu atapeleka umande wake wa uzima, nao wanaokuwa kwa wafu watatoka wazima.


Itakuja siku wazao wa Yakobo watatoa mizizi; watu wa Israeli watachanua na kuchipuka, na kuijaza dunia yote kwa matunda.


Litachanua maua kwa wingi kama waridi, litashangilia na kuimba kwa furaha. Mungu atalijalia utukufu wa milima ya Lebanoni, uzuri wa mulima Karmeli na wa bonde la Saroni. Watu watauona utukufu wa Yawe, watauona ukubwa wa Mungu wetu.


Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.


Enyi mbingu, munyeshe umande kutoka kule juu, mawingu yatiririshe ushindi; dunia ifuguke, ichipushe wokovu, na kuotesha haki vilevile! Mimi, Yawe nimefanya hayo.


Niliona mwenendo wao, lakini nitawaponyesha; nitawaongoza na kuwapa faraja, nitawatuliza hao wanaoomboleza.


Mimi nitawapa amani, amani kwa wanaokuwa mbali na wanaokuwa karibu! –Ni Yawe anayesema hivyo.– Mimi nitawaponyesha.


Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu, mimi nitawaponyesha ukosefu wenu wa uaminifu. Nanyi munasema: Sisi tunarudi kwako, maana wewe ndiwe Yawe, Mungu wetu.


Nitafurahi kuwatendea mema; nitawasimika siku zote katika inchi hii na kuwatendea kwa uaminifu.


Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.


Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima, wataenea kati ya mataifa na watu wengi watakuwa na nguvu kubwa kama simba kati ya nyama wa pori, kama simba mukali kati ya makundi ya kondoo, ambaye kila pahali anapopita, anarukia na kurarua nyama, na hakuna mutu yeyote wa kuiokoa.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


“Kwa sababu gani munajisumbua kwa ajili ya nguo? Muangalie maua jinsi yanavyoota. Hayatumiki wala kujisukia nguo.


Mufikiri juu ya namna maua yanavyoota. Hayasumbuki wala kujisukia nguo. Lakini ninawaambia kwamba hata mufalme Solomono katika utukufu wote aliokuwa nao, hakuvaa nguo inayoweza kulinganishwa na uzuri wa moja la maua.


Hivi Kristo apate kukaa ndani ya mioyo yenu kwa njia ya imani, nanyi mupate kuwa na mizizi na musingi katika upendo.


Mafundisho yangu yatone kama mvua, maneno yangu yadondoke kama umande, kama manyunyu kwenye mimea michanga, kama mvua nyepesi katika majani mabichi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ