Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 14:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Muombe huruma kwake, mumurudilie na kumwambia: Utusamehe uovu wote, upokee zawadi zetu, nasi tutakusifu kwa moyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 14:3
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa wakati ule, nabii Hanani akamwendea mufalme Asa wa Yuda, akamwambia: “Kwa sababu ulimutegemea mufalme wa Suria kuliko kumutegemea Yawe, Mungu wako, jeshi la mufalme wa Suria limekuponyoka.


Lakini wewe unawaona wenye taabu na shida; nawe uko tayari kuwasaidia siku zote. Muzaifu anakutegemea wewe, ee Mungu, wewe umekuwa siku zote musaada wa yatima.


Musiwategemee wakubwa wa dunia; hao ni wanadamu tu, hawawezi kuokoa.


Yawe anawalinda wageni, anawasaidia wajane na wayatima; lakini anaharibu mipango ya waovu.


Farasi wa vita hafai kitu kwa kupata ushindi; nguvu zake nyingi haziwezi kumwokoa mutu.


Mumwimbie Mungu, musifu jina lake; mumutengenezee njia yeye anayetembea juu ya mawingu. Jina lake ni Yawe; mufurahi mbele yake.


Mutapata haya kwa ajili ya miti ya mialo muliyoipenda sana; mutafezeheka kwa sababu ya bustani mulizofurahia.


Siku hiyo, watu watawatupia panya na popo sanamu za feza na zahabu walizojitengenezea kusudi waziabudu.


Hivi ndivyo uovu wa wazao wa Yakobo utakavyoondolewa, hivi ndivyo zambi yake itakavyofutwa kabisa: ataziharibu mazabahu za miungu; mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa. Sanamu za Ashera wala mazabahu za kufukizia ubani hazitabaki.


Pahali pake mulisema: Hapana! Sisi tutakimbia na farasi wenye mbio. Sawa, mutakimbia na farasi wenye mbio, lakini farasi wa waadui zenu wana mbio zaidi.


Bila kutaka shauri langu, wanafunga safari kwenda Misri, kukimbilia ulinzi kwa mufalme wa Misri, kupata pahali pa kujificha katika inchi yake.


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Wamisri ni wanadamu tu wala si miungu; farasi wao nao ni nyama tu, si roho. Yawe akiunyoosha mukono wake, taifa linalotoa musaada litajikwaa, na lile linalosaidiwa litaanguka; yote mawili yataangamia pamoja.


Basi, mufanye mapatano na bwana wangu mufalme wa Asuria. Mimi nitawapatia farasi elfu mbili, kama mutaweza kupata waaskari wapanda-farasi.


Muniachie watoto wenu wayatima nami nitawatunza; muwaache wajane wenu wanitegemee.


Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


Hawatajichafua tena kwa kuabudu sanamu za miungu yao na kwa mambo yao ya kuchukiza wala kwa makosa yao. Nitawaokoa wasikuwe tena waasi. Nao watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.


Watu wa Efuraimu wananizunguka kwa uongo, na Waisraeli kwa udanganyifu. Lakini watu wa Yuda wanaendelea kuwa mwaminifu kwa Mungu Mutakatifu.


Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!


Watarudi na kuishi chini ya ulinzi wangu, watastawi kama bustani nzuri. Watachanua kama muzabibu, harufu yao nzuri kama ya divai ya Lebanoni.


Huko nitamurudishia mashamba yake ya mizabibu. Bonde la Akori litakuwa mulango wa tumaini. Ataniitikia vizuri kama vile alipokuwa kijana, kama wakati alipotoka katika inchi ya Misri.


Watu wangu wanaomba shauri kutoka kwa muti; kijiti chao cha kuaguza ndicho kinachowapa shauri. Nia ya kufanya uzinzi imewapotosha; wamefanya uzinzi kwa kufuata miungu mingine, wakaniacha mimi Mungu wao.


Watu wa Efuraimu walipogundua ugonjwa wao, watu wa Yuda walipogundua kidonda chao, watu wa Efuraimu walikwenda Asuria kuomba musaada kwa mufalme mukubwa; lakini yeye hakuweza kuwatunza, hakuweza kuponyesha kidonda chao.


Efuraimu ni kama njiwa mujinga asiyekuwa na akili; mara yuko Misri, mara Asuria kwa kuomba musaada.


Ile sanamu inatoka Israeli, ni fundi ndiye aliyeitengeneza. Yenyewe si Mungu hata kidogo. Kweli! Sanamu ya mwana-ngombe ya Samaria itavunjwavunjwa!


Wamekwenda kuomba musaada Asuria. Efuraimu ni punda wa pori anayetangatanga peke yake; Efuraimu amejilipia wapenzi wake.


Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea sadaka, na kutimiza viapo vyangu. Yawe, ndiye anayeokoa.


Wakati ule, nitaondoa majina ya sanamu za miungu katika inchi, wala hayatakumbukwa tena. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondoa kabisa pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu.


“Sitawaacha kama wayatima, nitawarudilia tena.


Hata hivyo, asikuwe na farasi wengi kwa ajili yake mwenyewe, wala asiwarudishe watu Misri kwa kujipatia farasi zaidi, kwa sababu Yawe amewaonya: ‘Hamutarudi tena kwa njia ile.’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ