Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 13:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Nitawaangamiza, enyi Waisraeli. Nani ataweza kuwasaidia?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 13:9
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa sababu alitolea sadaka kwa miungu ya Damasiki iliyokuwa imemushinda katika vita akisema: “Kwa sababu miungu ya Suria iliwasaidia wafalme wa Shamu, nikiitolea sadaka labda itanisaidia nami vilevile.” Lakini ilisababisha kuangamia kwake na taifa lote la Israeli.


Heri mutu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo, mutu anayemutumainia Yawe, Mungu wake,


Mioyo yetu inamutumainia Yawe. Yeye ni musaidizi wetu na ngao yetu.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora: Kwa mutindo wa Sauti ya juu kabisa.


Anayezini hana akili kabisa; anajiangamiza yeye mwenyewe.


Asiyenipata anajizuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”


Lakini ole kwao watu waovu! Mambo yatawaendekea vibaya, maana yale waliyotenda yatawapata wao wenyewe.


Ubaguzi wao unashuhudia juu yao; wanatangaza zambi yao kama vile watu wa Sodoma, wala hawaifichi. Ole kwao watu hao, kwa sababu wamejiletea maangamizi wenyewe.


Israeli, si wewe mwenyewe uliyejiletea hayo yote, kwa kuniacha mimi Yawe, Mungu wako, niliyekuwa ninakuongoza katika njia?


Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–


Wewe Yuda, hayo yote yamekupata kwa ajili ya mwenendo na matendo yako. Hiyo ndiyo hasara inayokufikia, tena ni yenye uchungu; yamepenya mpaka ndani ya moyo wako.


Makosa yenu yamewazuia musipate baraka hizo, zambi zenu zimewafungia kupata mema yale.


Yawe anasema: Lakini mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri; hakuna mungu mwingine lakini mimi, wala hakuna anayeweza kuwaokoa.


Watu wa Samaria wataazibiwa kwa ajili ya kosa lao; wamemwasi Mungu wao. Watauawa kwa upanga, watoto wao watapondwapondwa, na wamama wenye mimba watapasuliwa tumbo.


Wananililia, lakini si kwa moyo. Wanagaagaa na kujikatakata juu ya vitanda vyao, kusudi nisikilize maombi yao kwa kupata ngano na divai; lakini wanaendelea kuniasi.


Mimi ndimi niliyeiimarisha mikono yao, lakini wanafikiri maovu juu yangu.


Lakini ninyi munalizarau jina langu pale munapoichafua mazabahu yangu, na chakula munachotoa juu yake munakizarau.


Munasema: Mambo haya yametuchokesha sana na munanizarau. Munaniletea sadaka za nyama muliopata kwa njia ya kunyanganya, au wanaokua vilema au wagonjwa. Basi, nipokee sadaka hizo toka katika mikono yenu?


Kwa hiyo sasa enyi makuhani, mumwombe Mungu kusudi atuhurumie. Yawe wa majeshi anasema hivi: Ikiwa munamutolea matoleo ya aina hiyo, kweli atawakubali?


Musa akamalizia kwa kusema: “Ee Israeli, hakuna anayekuwa kama Mungu wako, yeye anayeruka toka mbinguni kuja kukusaidia, anapita juu katika anga katika utukufu wake.


Heri yenu ninyi Waisraeli. Nani anayekuwa kama ninyi, watu muliookolewa na Yawe, ambaye ndiye ngao ya musaada wenu, na upanga unaowaletea ushindi! Waadui zenu watakuja wananyenyekea mbele yenu, nanyi mutawakanyaga chini.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ