12 Uovu wa Efuraimu uko umeandikwa, zambi yake imewekwa akiba.
Makosa yangu yangefungiwa katika mufuko, nawe ungefunika uovu wangu.
Ninyi munasema: “Mungu amewawekea watoto wao azabu ya watu wale waovu.” Kwa nini hawalipizi wao wenyewe, wapate kutambua?
Hata ukijisafisha kwa dawa ya kutosha taka na kutumia sabuni nyingi, madoa ya uovu wako yatabaki mbele yangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Lakini wewe ni mugumu na mwenye moyo usiotaka kugeuka. Kwa hiyo unajiwekea azabu kubwa siku Mungu atakapoonyesha kasirani yake na hukumu yake ya haki.