Kama watumishi wanavyomutegemea bwana wao, kama mujakazi anavyomutegemea bibi mukubwa wake, ndivyo nasi tunavyokutegemea wewe, ee Yawe, Mungu wetu, mpaka hapo utakapotuonea huruma.
Uwaambie Waisraeli kwamba: Yawe, Mungu wa babu zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutuma kwao. Hili ndilo jina langu milele, na hivi ndivyo nitakavyokumbukwa katika vizazi vyote.
Mafungo ninayotaka mimi ni haya: kuwafungua waliofungwa bila haki, kuziondoa kamba za utumwa, kuwaacha huru wanaogandamizwa, na kuvunja kabisa mambo yote ya kitumwa!
Unazani umekuwa mufalme kwa kujenga na mierezi? Baba yako alikula na kunywa, alifuata sheria yangu na kutenda mambo ya haki, na mambo yake yaliendeka vizuri.
Kwa hiyo, nitawahukumu ninyi Waisraeli, kila mumoja wenu, kulingana na mwenendo wake. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Mugeuke na kuachana na makosa yenu yasipate kuwaangamiza.
Watu wa Samaria wataazibiwa kwa ajili ya kosa lao; wamemwasi Mungu wao. Watauawa kwa upanga, watoto wao watapondwapondwa, na wamama wenye mimba watapasuliwa tumbo.
Musikilize maneno ya Yawe, enyi Waisraeli. Yawe anawashitaki wakaaji wa inchi hii. Hakuna tena uaminifu wala wema katika inchi; hakuna anayemujua Mungu katika inchi hii.
Munapasua nguo zenu kwa kuonyesha huzuni, lakini inafaa mioyo yenu ipasuke vilevile. Murudilie Yawe, Mungu wenu. Yeye amejaa huruma na rehema, hakasiriki upesi, ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia zake kusudi asiazibu.
Mungu ndiye aliyeifanya milima, na kuumba upepo; ndiye anayemujulisha mwanadamu mawazo yake; ndiye anayegeuza muchana kuwa usiku, na kukanyaga vilele vya dunia. Yawe wa majeshi ndilo jina lake!
Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.
Kwa hiyo muningojee mimi Yawe, ngoja siku nitakaposimama kutoa mashitaki. Nimeamua kuyakusanya mataifa na falme, kuyamwangia kasirani yangu, na ukali wa hasira yangu. Dunia yote itateketezwa kwa moto wa kasirani yangu.
Petro akawajibu: “Mugeuke toka katika zambi zenu, na kila mumoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo, na Mungu atawasamehe zambi zenu. Hivi mutapokea zawadi ya Roho Mutakatifu.
Lakini kwanza nilihubiri wakaaji wa Damasiki, na wa Yerusalema na wa jimbo lote la Yudea nao watu wa mataifa mengine vilevile. Nilihubiri kwao kwamba wageuke toka zambi zao na kumurudilia Mungu, nao waonyeshe kwa njia ya matendo yao kwamba wamegeuka.
Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.