Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 12:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yawe ana mashitaki juu ya Yuda; atawaazibu wazao wa Yakobo kadiri ya makosa yao, na kuwalipa kadiri ya matendo yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 12:3
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wa pili alizaliwa akiwa amemushika Esau kisigino, hivyo wakamupa jina Yakobo. Isaka alikuwa na umri wa miaka makumi sita wakati Esau na Yakobo walipozaliwa.


Basi, Yawe akawakasirikia sana watu wa Israeli na kuwafukuza kabisa mbele yake; hakuacha mutu isipokuwa kabila la Yuda peke yake.


Yawe aliwakataa Waisraeli wote; akawaazibu na kuwaacha katika mikono ya waadui wakali, na kisha akawafukuza mbele yake.


mpaka kwa mwisho Yawe akawafukuza kutoka mbele yake, kama vile alivyokuwa amesema kupitia kwa watumishi wake wote manabii. Kwa hiyo watu wa Israeli walipelekwa katika uhamisho kutoka katika inchi yao wenyewe mpaka Asuria ambako wanakaa hata sasa.


Kwa hiyo, mimi nitawashitaki ninyi, na nitawashitaki wazao wenu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Sasa mwisho umewafikia; sasa mutausikia ukali wa hasira yangu juu yenu. Nitawahukumu kufuatana na mwenendo wenu. Nitawaazibu kwa ajili ya machukizo yenu yote.


Sasa mutausikia uzito wa hasira yangu juu yenu. Nitawahukumu kulingana na mwenendo wenu; nitawaazibu kufuatana na machukizo yenu.


Musikilize maneno ya Yawe, enyi Waisraeli. Yawe anawashitaki wakaaji wa inchi hii. Hakuna tena uaminifu wala wema katika inchi; hakuna anayemujua Mungu katika inchi hii.


Lakini yatakayowapata watu yatawapata makuhani; nitawaazibu kwa sababu ya mwenendo wao, nitawalipiza matendo yao wenyewe.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Yuda, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamezarau sheria zangu, wala hawakufuata masharti yangu. Wamepotoshwa na miungu ileile babu zao waliyoifuata.


Musikilize mashitaki ya Yawe, enyi milima, musikilize enyi misingi imara ya dunia! Yawe yuko na maneno juu ya watu wake. Yeye atatoa mashitaki juu ya Waisraeli.


Watoto wale walipokuwa hawajazaliwa bado, wala hawajatenda jambo lolote zuri au baya, Mungu alimwambia Rebeka hivi juu yao: “Mukubwa atamutumikia mudogo.” Alisema vile kwa kutimiza mupango wake unaotokana na uchaguzi wake usiofuatana na matendo ya watu, lakini mwito wake kwao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ