Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 12:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kwa njia ya nabii, Yawe aliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri. Kwa njia ya nabii, Mungu aliwalinda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 12:14
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi akasema: “Ubebe wewe mwenyewe lazima ya kifo chako, maana umejishuhudia wewe mwenyewe kwa kinywa chako mwenyewe ukisema: ‘Nimemwua muchaguliwa wa Yawe.’ ”


Lakini ikiwa mutu huyo ana mutoto ambaye anafanya mabaya baba yake asiyofanya, yule mutoto atakufa kama anafanya machukizo haya: ananyanganya, anaua, anakula sadaka kwenye milima, anamuchafua muke wa jirani yake, anawatendea wamasikini na wakosefu vibaya, anaiba, harudishi rehani, anaangalia sanamu za miungu na kufanya machukizo, anakopesha kwa kupata faida na kujitafutia mazidio. Hakika atakufa, na yeye mwenyewe atabeba lazima ya kifo chake.


Maana aliisikia sauti ya baragumu, akazarau onyo; basi lawama itakuwa juu yake mwenyewe. Lakini kama angejali hilo onyo, angeyaokoa maisha yake.


Nyuma ya hayo, atageukia na kushambulia inchi nyingi za kandokando ya bahari na kuzishinda. Lakini jemadari mugeni atamushinda na kuyakomesha majivuno yake mwenyewe; kweli atamurudishia mufalme wa kaskazini majivuno yake mwenyewe.


Kuapa, uongo, mauaji, wizi na uzinzi vinatokea humo. Umwangaji wa damu unafuatana kwa mufululizo.


Wanaigeukia miungu ya bure, wako kama upinde ulioregea. Waongozi wao watakufa kwa upanga, kwa sababu ya maneno yao ya kiburi. Kwa hiyo, watazarauliwa katika inchi ya Misri.


Ninyi munafuata mufano mubaya wa mufalme Omuri na mufano mubaya wa jamaa ya mwana wake, Ahabu, na mumefuata mashauri yao. Kwa hiyo nitawaletea maangamizi, na kila mutu atawazarau. Watu watawachekelea kila pahali.


“Yawe, Mungu wenu atawachagulia nabii anayekuwa kama mimi kutoka kati yenu wenyewe, nanyi mutamutii huyo.


Nitawachagulia kati ya wandugu zao wenyewe nabii kama wewe, nitatia maneno yangu ndani ya kinywa chake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.


Nanyi mutakuwa kinyaa, mazarau na mushangao kati ya watu wote wa inchi ambako Yawe atawapeleka.


Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ