Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 12:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Watu wa Efuraimu wananizunguka kwa uongo, na Waisraeli kwa udanganyifu. Lakini watu wa Yuda wanaendelea kuwa mwaminifu kwa Mungu Mutakatifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 12:1
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu, nyuma ya hayo, masuke mengine saba membamba na yaliyokaushwa na upepo mukali wa jangwa yakatokea.


Basi, Puli mufalme wa Asuria akashambulia inchi ya Israeli, naye Menahemu akamupa kilo elfu makumi tatu na ine za feza kusudi amusaidie kuimarisha mamlaka yake juu ya inchi ya Israeli.


Tena alitengeneza pahali pa kuabudia miungu mingine katika milima ya Yuda na kusababisha wakaaji wa Yerusalema kukosa uaminifu na watu wa Yuda kupotoka.


Mwenye hekima anajibu bila kufikiri na kujaa maneno ya burebure?


Lakini walimudanganya kwa maneno yao; walimwambia uongo.


Kwa nini unaniachilia hivi, ukibadilishabadilisha mwenendo wako? Utafezeheshwa na Misri kama ulivyofezeheshwa na Asuria.


Waongozi wenu watapeperushwa na upepo, wapenzi wenu watapelekwa katika uhamisho. Halafu mutapata haya na kufazaika, kwa sababu ya uovu wenu wote.


Nitawafukuza ninyi mbali nami kama nilivyowatupilia mbali wandugu zenu, wote wa uzao wa Efuraimu.


Tumewanyooshea Wamisri na Waasuria mikono, kusudi tupate chakula cha kutosha.


Umepandikizwa, lakini, utastawi? Upepo mukali wa mashariki unapovuma juu yake utanyauka; utakaukia palepale kwenye udongo ulikoota.


Nitaizuia hasira yangu kali; sitamwangamiza tena Efuraimu, maana mimi ni Mungu, wala si mwanadamu. Mimi ndimi Mutakatifu kati yenu, nami sitakuja kuwaangamiza.


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


Basi, zoruba itawapeperusha, nao watapata haya kwa ajili ya sadaka zao.


Watu wa Efuraimu walipogundua ugonjwa wao, watu wa Yuda walipogundua kidonda chao, watu wa Efuraimu walikwenda Asuria kuomba musaada kwa mufalme mukubwa; lakini yeye hakuweza kuwatunza, hakuweza kuponyesha kidonda chao.


Kila mara nikitaka kurudishia watu wangu hali yao ya mbele, ninapotaka kuwaponyesha Waisraeli, uovu wa watu wa Efuraimu unafunuliwa, matendo mabaya ya Samaria yanajitokeza. Wao wanaongozwa na udanganyifu, mwizi anabomoa nyumba; inje katika barabara wanyanganyi wanashambulia.


Efuraimu ni kama njiwa mujinga asiyekuwa na akili; mara yuko Misri, mara Asuria kwa kuomba musaada.


Wanapanda upepo, watavuna zoruba! Mimea yao ya ngano inayokuwa katika mashamba haitatoa ngano yoyote. Na hata kama ikizaa, mazao yake yatakuliwa na wageni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ