Hosea 11:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20028 Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Lakini wakati malaika aliponyoosha mukono wake kuelekea Yerusalema kwa kuuangamiza, Yawe alibadilisha nia yake. Yawe akamwambia yule malaika aliyetimiza maangamizi kwa watu: “Basi! Inatosha; rudisha mukono wako.” Malaika wa Yawe alikuwa amesimama karibu na kiwanja cha kupepetea ngano cha Arauna wa muji wa Yebusi.
Yule mwanamuke aliyekuwa mama ya huyo mutoto anayekuwa muzima alishikwa na huruma juu ya mwana wake, akamwambia mufalme: “Tafazali mufalme, musimwue mutoto. Mumupe mwenzangu huyo mutoto mwenye kuwa muzima, amutwae yeye.” Lakini yule mwanamuke mwingine akasema: “Hapana! Mutoto asikuwe wangu wala wake. Mumukate vipande viwili.”
Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli– inchi ya Moabu itakuwa kama Sodoma na ya Amoni itakuwa kama Gomora. Inchi zake zitakuwa shamba la miiba na mashimo ya chumvi, zitakuwa ukiwa milele. Watu wangu watakaobaki wataziteka, watu wa taifa langu waliobaki watazirizi.