Hosea 11:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Mimi ndiye niliyemufundisha watu wa Efuraimu kutembea! Mimi mwenyewe niliwatwaa katika mikono yangu; lakini hawakutambua kwamba mimi ndiye niliyewatunza.
‘Ninyi wenyewe mumeona jinsi nilivyowatendea Wamisri na jinsi nilivyowapeleka ninyi kama vile tai anavyopeleka watoto wake kwa mabawa, nikawaleta kwangu.
Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwangaza wa jua utakuwa mara saba ya mwangaza wake wa kawaida, sawa vile kwamba mwangaza wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Yawe atakapofunga vidonda na kuponyesha mapigo aliyowaletea watu wake.
Musikilize, enyi wazao wa Yakobo, munisikilize, enyi mabaki ya watu wangu wa Israeli. Mimi niliwatunza ninyi tangu mulipozaliwa; niliwabeba ninyi tangu katika tumbo la mama yenu.
Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.
Sasa wanakuita wewe Sayuni: “Aliyetupiliwa”, “Muji usioshugulikiwa na mutu”. Lakini nitakurudishia afya yako, nitaponyesha vidonda vyako. –Ni ujumbe wa Yawe.
Inchi ya Asuria haitatuokoa, hatutategemea tena farasi wa vita. Hatutaziita tena Mungu wetu hizo sanamu tulizochonga. Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma.
Kila mara nikitaka kurudishia watu wangu hali yao ya mbele, ninapotaka kuwaponyesha Waisraeli, uovu wa watu wa Efuraimu unafunuliwa, matendo mabaya ya Samaria yanajitokeza. Wao wanaongozwa na udanganyifu, mwizi anabomoa nyumba; inje katika barabara wanyanganyi wanashambulia.
Mukumbuke jinsi Yawe, Mungu wenu, alivyowaongoza katika safari ndefu kupitia katika jangwa kwa muda wa miaka hiyo makumi ine, kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kusudi ajue yanayokuwa ndani ya mioyo yenu, na kama mungeshika amri zake au hapana.