Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.
Watakuja na kuimba kwa sauti juu ya mulima Sayuni, watapata utukufu juu ya wema wangu mimi Yawe, kwa ajili ya ngano, divai na mafuta ninavyowapa, kwa ajili ya kondoo na ngombe vilevile; maisha yao yatakuwa kama bustani iliyotiliwa maji, wala hawataregea tena.
Miti inayokuwa katika mashamba itazaa matunda, udongo utatoa mazao kwa wingi, nao wataishi kwa salama katika inchi yao. Nitakapovunja nira zao za utumwa na kuwaokoa toka katika mikono ya hao waliowafanya kuwa watumwa halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitawatoa Waisraeli kutoka mataifa walikokwenda; nitawakusanya toka pande zote na kuwarudisha katika inchi yao.
Watakaa katika inchi ya wazee wao ambayo nilimupa Yakobo. Wao na watoto wao na wajukuu wao wataishi humo milele. Naye Daudi, mutumishi wangu, atakuwa mutawala milele.
Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho.
Lakini wale waliobaki watakaa kwa mulima Sayuni nao utakuwa mulima mutakatifu. Wazao wa Yakobo watanyanganya inchi yao toka kwa wale waliokuwa wameinyanganya.
Nitawarudisha kutoka inchi ya Misri, nitawakusanya kutoka Asuria; nitawaleta katika inchi ya Gileadi na Lebanoni, nao watajaa kila nafasi katika inchi.