Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 11:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Watanifuata mimi Yawe ninayenguruma kama simba; nitakaponguruma watanifikia toka magaribi wakitetemeka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 11:10
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kutokana na hayo, moyo wangu unatetemeka, na kuruka kutoka pahali pake.


Ninatetemeka kwa kukuogopa wewe; nimejaa hofu kwa sababu ya maamuzi yako.


Mumutumikie Yawe kwa woga; muiname mbele ya mwana wake na kutetemeka, kusudi asikasirike, nanyi musiangamie kwa rafla; kwa maana hasira yake inawaka haraka. Heri wote wanaokimbilia kwake!


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


Sasa, enyi wazao wa Yakobo, mukuje, tutembee katika mwangaza wa Yawe.


Yawe aliniambia hivi: Simba mukali ananguruma kwa kukinga nyama aliyemukamata; hata kundi la wachungaji likiitwa kwa kumufukuza, hatishiki kwa kelele zao, wala hashituki kwa sauti zao. Ni vile Yawe wa majeshi atakavyoshuka kupigana juu ya mulima Sayuni na kilima chake.


Yawe anajitokeza kama shujaa; kama vile askari katika vita anatatanua kupigana. Anapiga kelele kubwa la vita na kujionyesha mwenye nguvu juu ya waadui zake.


Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.


Wakati ulipotenda maajabu ambayo hatukutazamia, ulishuka chini nayo milima ikatetemeka ilipokuona.


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Musikilize neno la Yawe, enyi munaotetemeka kwa sababu ya neno lake. Wandugu zenu ambao wanawachukia, na kuwafukuza kwa sababu yangu, wamesema hivi kwa kuwachekelea: Mungu aonyeshe utukufu wake, nasi tuwaone ninyi mukishinda! Lakini wao wenyewe ndio watakaopata haya!


Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.


Basi, wewe Yeremia utatabiri maneno haya yote juu yao, na kusema hivi: Yawe atanguruma kutoka juu, atatoa sauti yake kutoka kwenye makao yake matakatifu; atanguruma kwa nguvu kwa ajili ya watu wake, atapiga kelele kama wenye kukamua zabibu, kwa ajili ya wakaaji wote wa dunia.


Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.


Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.


Mbona hamuniogopi? –Ni ujumbe wa Yawe.– Kwa nini hamutetemeki mbele yangu? Mimi niliwekea bahari muchanga kuwa mupaka wake; ni kizuizo cha milele ambacho bahari haiwezi kuvuka. Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita; ingawa yanavuma, hayawezi kuuruka.


Siku hizo na wakati huo, watu wa Israeli na watu wa Yuda watakusanyika pamoja na kuja wakilia na kutafuta Yawe, Mungu wao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Musiwatese wageni, wayatima au wajane au kuwaua watu wasiokuwa na kosa katika inchi hii. Musijiangamize wenyewe kwa kuabudu miungu mingine.


Munaiba, munaua, munafanya uzinzi, munaapa kwa uongo, munamufukizia mungu Bali ubani na kuabudu miungu mingine ambayo hamujapata kuijua.


Wakubwa wote wa mataifa ya kandokando ya bahari watashuka toka kwenye viti vyao vya kifalme, na kuvua nguo zao za heshima pamoja na nguo zao zilizopindwa. Kisha kujaa hofu, wataikaa chini; nao watatetemeka wakati wote na kushangaa sana juu ya hayo yaliyokupata.


Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho.


Amosi alisema hivi: Yawe ananguruma toka mulima Sayuni, anavumisha sauti yake toka Yerusalema, hata mashamba ya malisho ya wachungaji yanakauka, majani ya mulima Karmeli yananyauka.


Simba ananguruma katika pori kama hajapata nyama? Simba mukali ananguruma katika pango lake kama hajakamata kitu?


Simba akinguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana wetu Yawe akisema, ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?


Mataifa mengine yanafuata njia zao, kwa kuitegemea miungu yao, lakini sisi tunafuata njia zetu kwa kumutegemea Yawe, Mungu wetu, milele na milele.


Nikasikia hayo, matumbotumbo yangu yakatetemeka. Midomo yangu inatetemeka kwa hofu, mifupa yangu inateguka, miguu yangu inatetemeka. Ninangojea kwa utulivu siku ile ya hasara, ambayo inawafikia wale wanaotushambulia.


Nitawarudisha kutoka inchi ya Misri, nitawakusanya kutoka Asuria; nitawaleta katika inchi ya Gileadi na Lebanoni, nao watajaa kila nafasi katika inchi.


Mimi nitawaimarisha watu wangu, nao watanitii na kuishi kwa kunipendeza. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Yawe anasema hivi: Nitawaokoa watu wangu kutoka inchi ya mashariki na kutoka inchi ya magaribi


Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


Lakini Paulo alipokuwa akihubiri juu ya haki, juu ya kujizuiza na juu ya siku ya hukumu ya Mungu itakayokuja, Feliki akaogopa na kumwambia: “Kwa sasa unaweza kujiendea. Nitakuita tena nitakapopata wakati.”


Basi sasa hakuna azabu kwa wale wanaoungana na Yesu Kristo.


Na zaidi atawaazibu wale wanaoishi kufuatana na tamaa mbaya za kimwili na kuzarau mamlaka ya Mungu. Walimu wale wa uongo ni wenye kiburi, wenye kujivuna, nao hawaogopi kutukana viumbe vitukufu vya mbinguni.


Akalalamika kwa sauti kubwa kama simba anayenguruma. Na alipokwisha kulalamika, kukasikilika mulio wa ngurumo saba ya radi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ