Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 10:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Pahali pa kutambikia juu ya vilima pa Aweni, pahali Waisraeli walipofanyia zambi, pataharibiwa. Miiba na michongoma vitaota katika mazabahu zao. Nao wataiambia milima: Mutufunike na vilima: Mutuangukie!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 10:8
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Magaribi mwanaume na muke wake wakasikia Yawe Mungu akitembea katika bustani, nao wakajificha kati ya miti ya bustani, Yawe Mungu asipate kuwaona.


Mutu huyo akailaani ile mazabahu akisema: “Ee mazabahu, Yawe anasema hivi: ‘Kutazaliwa mutoto katika ukoo wa Daudi, jina lake Yosia. Huyo atawatwaa makuhani wanaotumika kwa nafasi ya ibada na kufukiza ubani juu yako, na kuwatambika juu yako. Hakika, mifupa ya watu itateketezwa juu yako!’ ”


Tendo hili likakuwa zambi ambayo ilisababisha ukoo wa Yeroboamu ufutiliwe mbali na kuangamizwa.


Yawe ataitupilia Israeli kwa sababu ya zambi za Yeroboamu ambaye alitenda zambi na kuwasukuma watu wa Israeli vilevile watende zambi.”


Zaidi ya hayo aliharibu kule Beteli pahali pa kuabudia palipojengwa na mufalme Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Aliharibu mazabahu hayo na kuvunja mawe yake vipandevipande, na kisha akaviponda mpaka vikakuwa mavumbi. Vilevile akachoma sanamu ya Ashera.


Nyuma ya sherehe kumalizika, watu wote wa Israeli wakakwenda katika kila muji wa Yuda, wakavunjavunja nguzo za mawe na kukatakata sanamu za Ashera, mungu wa kike, na vilevile wakaharibu mazabahu na pahali pa kuabudia miungu mingine. Wakafanya vile katika inchi yote ya Yuda, Benjamina, Efuraimu na Manase, mpaka walipokwisha kuvimaliza vyote. Kisha Waisraeli wakarudi kwao, kila mutu kwenye urizi wake.


Muingie katika mapango chini ya mawe, katika mashimo ndani ya udongo, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake, atakapokuja kuogopesha dunia.


Nao wataingia katika mapango chini ya mawe na kwenye nyufa za mawe, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake, atakapokuja kuogopesha dunia.


juu ya inchi ya watu wangu inayoota miiba na michongoma, juu ya nyumba zote zilizojaa watu wenye furaha, juu ya muji uliokuwa na shangwe.


Miiba itaota katika pango zake, miiba na michongoma ndani ya kuta zake. Itakuwa makao ya imbwa wa pori, nafasi ya mbuni.


Mioyo yao imejaa udanganyifu. Sasa ni lazima wabebe makosa yao. Yawe atabomoa mazabahu zao na kuziharibu nguzo zao.


Wakaaji wa Samaria watatetemeka kwa sababu ya sanamu ya mwana-ngombe wa kule Beteli. Watu wake watamwombolezea mwana-ngombe yule, hata makuhani wanaomwabudu watamulilia; maana utukufu wa mwana-ngombe yule umeondolewa.


Enyi Waisraeli, ninyi mumetenda zambi tangia kule Gibea, na mpaka sasa munaendelea. Hakika vita itawaangamizia kulekule Gibea.


Na watoto wake sitawahurumia, maana ni watoto wa uzinzi.


Wanatambikia kwenye vilele vya milima; wanatoa sadaka kwenye vilima, chini ya miti ya mwalo, migude na mikwaju, maana kivuli chao ni kizuri. Kwa hiyo wabinti wenu wanafanya uzinzi, na bibi-arusi wenu anafanya uasherati.


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


Mupige baragumu kule Gibea, na ngunga kule Rama. Mupige kelele la kujulisha hatari kule Beti-Aweni. Enyi watu wa Benjamina, adui yenu yuko nyuma!


Enyi watu wa Samaria, ninaichukia sanamu yenu ya mwana-ngombe. Hasira yangu inawaka juu yenu. Mutaendelea kuwa na makosa mpaka wakati gani?


Mutakapoyakimbia maangamizi ya inchi yenu, Misri itawakaribisha ninyi kwake, lakini makaburi yenu yanawangoja kule Memufisi. Michongoma itaota katika vyombo vyenu vya feza, miiba itajaa katika mahema yenu.


Nitavivunjavunja vifungio vya milango ya muji wa Damasiki, na kuwaondoa wakaaji wa bonde la Aweni, pamoja na mutawala wa Beti-Edeni. Waaramu wanapelekwa katika uhamisho kule Kiri. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.


Kule kwenye vilima ambapo wazao wa Isaka wanatambikia, kutafanywa kuwa uharibifu mutupu na mahekalu ya Waisraeli yatakuwa mabomoko. Nitaushambulia kwa vita ukoo wa mufalme Yeroboamu.


Wale wanaoapa kwa mungu wa uongo wa Samaria na kusema “Kwa nafsi ya mungu wako ee Dani” au “Kwa nafsi ya mungu wa Beri-Seba”, wote wataanguka na hawatasimama tena hata kidogo.


Enyi wakaaji wa Lakisi, mufunge farasi wepesi na magari ya vita. Ninyi mulikuwa mumeiga zambi ya watu wa Sayuni, makosa ya Waisraeli yalikuwa kwenu.


Haya yote yatatukia kwa sababu ya makosa ya wazao wa Yakobo, kwa sababu ya zambi za wazao wa Israeli. Kosa la Yakobo linaonekana wapi? Katika muji wake mukubwa Samaria! Kosa la Yuda linaonekana wapi? Katika Yerusalema kwenyewe!


Ninawe, nawe vilevile utalewa; utamukimbia adui na kujaribu kujificha.


Wakati ule watu wataanza kuiambia milima ‘Mutuangukie’, navyo vilima ‘Mutufunike!’


Kile kitu kiovu, ni kusema yule mwana-ngombe muliyejitengenezea, nilikitwaa, nikakiteketeza ndani ya moto, nikakipondaponda na kukisagasaga, kikakuwa mavumbi laini. Halafu nikayatupa hayo mavumbi kwenye kijito kilichotiririka chini ya mulima huo.


Nao wakaiambia milima na mawe: “Mutuangukie na kutufunika mbali na yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme na mbali na kasirani ya Mwana-Kondoo.


Na kwa muda ule, watu watatafuta kifo, lakini hakitawapata. Watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ