Lakini malaika wa Yawe akamwambia nabii Elia wa muji wa Tisibe, aende kukutana na wajumbe hao na kuwauliza: “Kwa nini munakwenda kwa Bali-Zebubu, mungu wa Ekuroni? Hakuna Mungu katika inchi ya Israeli?
Katika mwaka wa makumi mbili wa utawala wa Yotamu mwana wa Uzia mufalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela alimwasi Peka mwana wa Remalia na kumwua, kisha akatawala kwa pahali pake.
Lakini wakati mumoja Hoshea alituma wajumbe kwa mufalme wa Misri akiomba musaada; ndipo akaacha kulipa kodi kwa mufalme Salmanaseri wa Asuria kama vile alivyozoea kufanya kila mwaka. Salmanaseri alipoona hivi alimufunga Hoshea kwa minyororo na kumuweka katika kifungo.
Pahali pa kutambikia juu ya vilima pa Aweni, pahali Waisraeli walipofanyia zambi, pataharibiwa. Miiba na michongoma vitaota katika mazabahu zao. Nao wataiambia milima: Mutufunike na vilima: Mutuangukie!
Wanafanana na zoruba kubwa ya bahari na matendo yao ya haya yanaonekana kama pofu ya zoruba. Wanafanana vilevile na nyota zinazotangatanga; Mungu amekwisha kuwawekea nafasi katika giza kubwa kwa milele.