Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 10:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Sanamu hiyo itapelekwa Asuria, kama zawadi kwa mufalme mukubwa. Watu wa Efuraimu watafezeheka, Waisraeli watapata haya kwa ajili ya sanamu yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 10:6
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Salmanaseri wa Asuria alimushambulia; naye Hoshea akakuwa mutumishi wake na kumulipa kodi.


Hatua zake ndefu zitafupishwa; mipango yake itamwangusha chini.


Mutapata haya kwa ajili ya miti ya mialo muliyoipenda sana; mutafezeheka kwa sababu ya bustani mulizofurahia.


Lakini ulinzi wa Mufalme wa Misri utakuwa haya yenu, na kujificha katika inchi ya Misri kutakuwa fezeha yenu.


Watengenezaji wa sanamu watapata haya na kuzarauliwa, wote pamoja watafezeheka.


Halafu Wamoabu watapata haya kwa ajili ya mungu wao Kemosi, kama vile watu wa Israeli walivyopata haya kwa ajili ya kutegemea Beteli.


Lakini wao hawakunitii wala kunitegea sikio. Lakini wakafuata mashauri yao wenyewe na ugumu wa mioyo yao, wakarudi nyuma pahali pa kusonga mbele.


Kwa sababu haukutosheka, ulifanya tena uzinzi na Waasuria. Na hiyo vilevile haikukutoshelea.


Kisha mutakapokumbuka mienendo yenu miovu na matendo yenu mabaya, mutajichukia wenyewe kwa sababu ya maovu yenu na machukizo muliyofanya.


Atabeba sanamu za miungu yao na vyombo vya bei kali vya feza na zahabu mpaka katika inchi ya Misri. Kwa muda wa miaka michache, mufalme wa kusini hatamushambulia mufalme wa kaskazini.


Basi, zoruba itawapeperusha, nao watapata haya kwa ajili ya sadaka zao.


Kadiri makuhani walivyoongezeka, ndivyo wote walivyozidi kuniasi. Basi, nitageuza utukufu wao kuwa haya.


Watu wa Efuraimu walipogundua ugonjwa wao, watu wa Yuda walipogundua kidonda chao, watu wa Efuraimu walikwenda Asuria kuomba musaada kwa mufalme mukubwa; lakini yeye hakuweza kuwatunza, hakuweza kuponyesha kidonda chao.


Ile sanamu inatoka Israeli, ni fundi ndiye aliyeitengeneza. Yenyewe si Mungu hata kidogo. Kweli! Sanamu ya mwana-ngombe ya Samaria itavunjwavunjwa!


Ninyi munafuata mufano mubaya wa mufalme Omuri na mufano mubaya wa jamaa ya mwana wake, Ahabu, na mumefuata mashauri yao. Kwa hiyo nitawaletea maangamizi, na kila mutu atawazarau. Watu watawachekelea kila pahali.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ