Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!
Farasi wanaweza kukimbia katika mawe makubwa? Watu wanaweza kulima bahari na ngombe? Lakini ninyi mumeigeuza sheria kuwa sumu, na tunda la haki kuwa uchungu.
Kisha kusikia maneno ya agano hili ambayo mumeapishwa, na mutu akijiamini mwenyewe ndani ya moyo wake na kusema atakuwa salama naye akifuata ugumu wake, hiyo italeta maangamizi.
Yawe akamwambia Musa: “Umekaribia sasa kuaga dunia, na kisha kufa kwako, watu wataanza kuniacha na kuendea miungu mingine ya inchi hiyo ambamo watakwenda kuishi. Wataniacha na kuvunja agano nililoagana nao.
Hapo hasira yangu itawawakia siku hiyo, nami nitawaacha na kuficha uso wangu mbali nao, wataangamizwa. Maovu mengi na taabu zitawapata hata watambue kwamba maovu hayo yamewapata kwa sababu Mungu wao hayuko kati yao.
Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi.