Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 10:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Efuraimu ni mwana-ngombe aliyefundishwa vizuri, akapenda kupepeta ngano. Lakini sasa shingo yake nzuri nitaifunga nira. Yuda atalima kwa jembe yeye mwenyewe, Yakobo atakokota jembe la kupalilia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 10:11
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mulimaji anayetaka kupanda mbegu anaendelea kulima tu siku zote? Anaendelea kutipua na kusawanisha shamba lake?


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimeweka nira ya chuma ya utumwa kwenye shingo la mataifa yote ya pande hizi, yakuwe katika utumwa, nayo yatamutumikia Nebukadneza, mufalme wa Babeli. Nimemupa Nebukadneza hata nyama wa pori wamutumikie.


Misri ni kama mwana-ngombe muzuri, lakini uharibifu kutoka kaskazini umekuja juu yake.


Enyi wanyanganyi wa mali yangu, ijapokuwa munafurahi na kushangilia, munarukaruka kama mwana-ngombe anayepepeta ngano, na kulia kama farasi dume,


Niliwaongoza kwa huruma, nilishikamana nao kwa upendo; kama baba anavyomunyanyua mutoto mpaka kwenye shavu lake, ndivyo nami nilivyokuwa kwao. Mimi niliinama chini na kuwakulisha.


Kama sivyo, nitamuvua nguo abaki uchi, nitamufanya akuwe sawa vile alivyozaliwa. Nitamufanya akuwe utupu sawa jangwa, akauke sawa inchi kavu. Nitamwua kwa kiu.


Yawe akaniambia: Kwenda tena umupende mwanamuke anayependwa na mwanaume mwingine na ambaye ni muzinzi. Umupende kama vile mimi Yawe ninavyowapenda Waisraeli, ingawa wao wanaigeukia miungu mingine na kupenda mikate ya zabibu.


Waisraeli ni wenye kichwa kigumu kama punda. Kwa nini basi Mungu ashugulike na kuwachunga, kama kondoo katika shamba kubwa la kuwakulishia?


Musifurahi enyi Waisraeli! Musishangilie kama watu wa mataifa mengine; maana, mumekuwa wazinzi kwa kumwacha Mungu wenu. Mumefurahia malipo ya uzinzi, kwa kila nafasi ya kupepetea ngano.


Yawe anasema: Enyi watu wa Sayuni, musimame muwakanyagekanyage! Nitawapatia nguvu kama ngombe dume mwenye pembe za chuma na kwato za shaba. Mutawasaga watu wa mataifa mengi; mutanitolea mimi mapato yao, mutanitolea mali zao mimi Bwana wa dunia yote.


Kwa maana watu wa namna hii hawamutumikii Bwana wetu Kristo, lakini wanatumikia tu tumbo yao wenyewe. Tena kwa maneno yao matamu na ya kujipendekeza wanadanganya watu wasiokuwa na makosa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ