Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 1:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Gomeri alipata mimba tena, akazaa mutoto mwanamuke. Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Asiyehurumiwa”, maana sitawahurumia tena Waisraeli wala sitawasamehe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 1:6
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe aliwakataa Waisraeli wote; akawaazibu na kuwaacha katika mikono ya waadui wakali, na kisha akawafukuza mbele yake.


Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mufalme wa Asuria aliuteka muji wa Samaria na kuwapeleka watu wa Israeli katika uhamisho mpaka Asuria. Wamoja kati yao akawaweka katika muji wa Hala, wengine karibu na muto Habori, muto Gozani na wengine katika miji ya Wamedi.


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Gomeri alipomwachisha yule binti wake Asiyehurumiwa kunyonya, alipata mimba tena, akazaa mutoto mwingine mwanaume.


Siku hiyo, nitajibu kwa mahitaji ya mbingu ya kunyesha mvua, mbingu nazo zitajibu kwa mahitaji ya udongo. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mumushitaki mama yenu, mumushitaki, maana sasa yeye si muke wangu wala mimi si mume wake. Mumushitaki aondoe vitambulisho vya uasherati juu ya uso wake, ajiepushe na mapambo ya uzinzi juu ya kifua chake.


Naye akaniuliza: Amosi, unaona nini? Nikamujibu: Ninaona timazi. Kisha Yawe akasema: Ninaweka timazi kati ya watu wangu Waisraeli. Sitavumilia tena maovu yao.


Ninauangalia ufalme wenye zambi, na nitauangamiza kabisa kutoka katika dunia. Lakini sitawaangamiza wazao wote wa Yakobo. –Ni ujumbe wa Yawe.


Zamani ninyi hamukukuwa watu wa Mungu, lakini sasa munakuwa watu wake; zamani ninyi hamukuhurumiwa na Mungu, lakini sasa mumehurumiwa naye.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ