Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe alipoanza kusema na Waisraeli kwa njia ya Hosea, alimwambia hivi: Kwenda kuoa mwanamuke muzinzi, uzae naye watoto wa uzinzi, maana watu wa inchi hii wanafanya uzinzi mwingi kwa kuniacha mimi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 1:2
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini umeifuata mienendo ya wafalme wa Israeli na kuwaongoza watu wa Yuda na wa Yerusalema katika kukosa uaminifu kama vile Ahabu, na wafalme wa jamaa yake waliomufuata walivyoongoza Israeli kukosa uaminifu. Vilevile umewaua wandugu zako, wandugu za baba mumoja waliokuwa watu wema zaidi kuliko wewe.


Hivyo wakajichafua kwa matendo yao, wakakosa uaminifu kwa Mungu kama wazini.


Anayejitenga nawe, hakika ataangamia. Anayekukana, utamwangamiza.


Watu wangu wametenda maovu mawili; wameniacha mimi ninayekuwa chemichemi ya maji ya uzima, wakajichimbia visima vyao wenyewe, visima vyenye nyufa, visivyoweza kuchunga maji.


Yawe anasema: Tangu zamani wewe ulivunja nira yako, ulikata minyororo yako, ukasema: “Sitakutumikia”. Juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wa majani mabichi, ukalala machali kama kahaba.


Namna gani basi unaweza kusema: Mimi sikujichafua wala sikufuata miungu Bali. Ukumbuke vile ulivyotenda zambi kule katika bonde; utambue yale uliyofanya huko! Wewe ni kama mwana wa ngamia, anayetangatanga huko na huko;


Aliona kwamba ukahaba ni jambo dogo sana kwake. Aliichafua inchi kwa kufanya ukahaba, akiabudu mawe na miti.


Halafu wale walioponyoka watanikumbuka katikati ya mataifa ambamo watakuwa wamepelekwa katika uhamisho. Nitakuwa nimewavunja moyo wao wa uzinzi ambao ulinitupilia mbali, na macho yao yaliyozini na sanamu zao. Kwa hiyo watajichukia wao wenyewe kwa sababu ya maovu na machukizo yao yote waliyoyatenda.


Mama yao amefanya uzinzi, aliyebeba mimba yao amefanya mambo ya haya. Alisema: Nitaambatana na wapenzi wangu, ambao wananipatia chakula na maji, nguo za sufu na kitani, pamoja na mafuta na divai.


Yawe akaniambia: Kwenda tena umupende mwanamuke anayependwa na mwanaume mwingine na ambaye ni muzinzi. Umupende kama vile mimi Yawe ninavyowapenda Waisraeli, ingawa wao wanaigeukia miungu mingine na kupenda mikate ya zabibu.


Ninawajua watu wa Efuraimu, Waisraeli hawakufichwa kwangu. Ninyi watu wa Efuraimu mumefanya uzinzi, watu wote wa Israeli wamejichafua.


Huu ndio mwanzo wa Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.


Yawe akamwambia Musa: “Umekaribia sasa kuaga dunia, na kisha kufa kwako, watu wataanza kuniacha na kuendea miungu mingine ya inchi hiyo ambamo watakwenda kuishi. Wataniacha na kuvunja agano nililoagana nao.


Macho yao yanajaa uzinzi. Wao hawachoki kufanya zambi. Wanavuta watu wasiokamilika. Wanatawaliwa na tamaa za kupata mali. Watu hao wamelaaniwa!


Alikuwa ameandikwa juu ya paji la uso wake jina lenye fumbo: “Muji mukubwa Babeli, mama ya washerati na machukizo ya dunia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ