Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 9:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Lakini, watu wamoja waliokuwa pale walikuwa hawawezi kushiriki sikukuu hiyo ya Pasaka kwa sababu walikuwa wamegusa maiti, wakakuwa wachafu. Hao waliwaendea Musa na Haruni,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 9:6
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Musa akamujibu baba mukwe wake: “Kwa sababu watu wanakuja kwangu kuuliza mapenzi ya Mungu.


Sikiliza shauri langu kwako na Mungu akuwe pamoja nawe. Wewe utawasimamia watu mbele ya Mungu na kumuletea Mungu matatizo yao.


Nao wakakuwa wanaamua matatizo ya watu kila wakati. Matatizo magumu walimuletea Musa, lakini yale madogomadogo waliyatatua wao wenyewe.


Asikaribie maiti wala kujichafua kwa maiti hata kama ni ya baba yake au ya mama yake.


Yule kijana ambaye mama yake aliitwa Selemoti binti ya Dibri wa kabila la Dani, alitukana Mungu na kuzarau jina lake. Basi watu wakamupeleka kijana kwa Musa,


Basi, mutu huyo akapelekwa mbele ya Musa, Haruni na Waisraeli wengine wote.


Mutu akigusa maiti ya mutu yeyote, atakuwa muchafu kwa siku saba.


Na hii ndiyo sheria ya kufuatwa kama mutu akikufia ndani ya hema: Kila mutu atakayeingia ndani ya hema hilo, au aliyekuwa ndani ya hema hilo, atakuwa muchafu kwa siku saba.


Mutu yeyote akigusa mwili wa mutu aliyeuawa au aliyekufa kifo cha kawaida inje ya nyumba, au akigusa mufupa wa mutu au kaburi, atakuwa muchafu kwa siku saba.


Mutu anayekuwa safi atatwaa hisopo, halafu ataichovya katika maji hayo, kisha atainyunyizia hema, vyombo vyote vinavyokuwa ndani ya hema na watu wanaokuwa ndani. Atamunyunyizia vilevile mutu aliyegusa mufupa wa mutu, au mwili wa mutu aliyeuawa au aliyekufa kifo cha kawaida, au aliyegusa kaburi.


Basi, hao wabinti wane wakamwendea Musa, wakasimama mbele yake na kuhani Eleazari na viongozi wote wa Waisraeli, kwenye mulango wa hema la mukutano, wakasema:


Musa akaleta malalamiko yao mbele ya Yawe.


Uwaamuru Waisraeli wamutoe inje ya kambi kila mutu mwenye ukoma, kila mutu anayetokwa usaha, na kila anayekuwa muchafu kwa kugusa maiti.


wakawaambia: Sisi tuko wachafu kwa sababu tumegusa maiti, lakini kwa nini tukatazwe kumutolea Yawe sadaka zake kwa wakati uliopangwa pamoja na Waisraeli wengine?


Na kulipokucha asubui mapema, wakamutosha Yesu kwa Kayafa na kumupeleka kwenye nyumba ya liwali. Lakini Wayuda wenyewe hawakuingia ndani ya nyumba ya liwali, kwa maana kwa njia ile wangejichafua na kutoweza kuwa tayari kula karamu ya Pasaka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ