Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 9:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Ikiwa ni siku mbili, mwezi, mwaka au zaidi, muda wote wingu hilo lilipokuwa juu ya hema, Waisraeli hawakuhama; lakini lilipoinuliwa, nao vilevile walihama.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 9:22
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Aliwaongoza katika njia iliyonyooka, mpaka wakafika katika muji wa kukaa.


Unifundishe kutimiza mapenzi yako, maana wewe ni Mungu wangu! Roho wako muzuri aniongoze katika njia sawa.


Mungu anasema: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayofuata. Nitakushauria kwa uangalifu mukubwa.


Muangalie kuta zake na kuchunguza pango zake za kukimbilia, mupate kuelezea vizazi vitakavyokuja kwamba:


Wewe unaniongoza kwa mashauri yako; na kwa mwisho utanipokea kwenye utukufu.


Wewe ukajifanyia njia juu ya bahari; ulitembea juu ya maji yale mengi, lakini pahali ulipopita hapakuonekana.


Waisraeli walifanya kila kitu kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Basi, Musa alitimiza kwa ukamilifu kabisa maagizo yote ya Yawe.


Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Kwa hiyo Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja wakatakasa Walawi, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Kila mara wingu hilo lilipoinuliwa juu ya hema, Waisraeli walivunja kambi na kupiga kambi tena pahali wingu hilo lilipotua.


Wakati mwingine wingu lilikaa juu ya hema tangu magaribi mpaka asubui tu; na mara tu lilipoinuliwa, hao watu vilevile walifunga safari. Na ikiwa lilikaa juu ya hema muchana kutwa na usiku kucha, wao waliondoka tu wingu lilipoinuliwa.


Siku moja alipokuwa akikusanyika pamoja nao, akawaagiza: “Musitoke Yerusalema, lakini mubaki kule mukingojea zawadi ambayo Baba yangu aliahidi, ile niliyowaambia ninyi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ