Utawachagua wakuwe waangalizi wa hema la kuchunga vibao vya agano, vyombo vyake vyote na kila kitu kinachokuwa ndani yake; watakuwa wakilibeba pamoja na vyombo vyake vyote. Watatumika mule ndani na watapiga kambi yao kwa kulizunguka.
na nimewatoa kwa Haruni na wana wake, kama vile zawadi kutoka kwa Waisraeli, kusudi wafanye kazi katika hema la mukutano kwa ajili ya Waisraeli na kuwafanyia upatanisho kusudi kusitokee pigo kati ya Waisraeli wakikaribia Pahali Patakatifu.
Walawi wakajitakasa zambi na kufua nguo zao, naye Haruni akawatoa kama vile sadaka ya kutikiswa mbele ya Yawe. Vilevile, Haruni akafanya upatanisho kwa ajili yao kwa kuwatakasa.
Ikiwa ni siku mbili, mwezi, mwaka au zaidi, muda wote wingu hilo lilipokuwa juu ya hema, Waisraeli hawakuhama; lakini lilipoinuliwa, nao vilevile walihama.
Basi, wakafanya Pasaka magaribi, siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza, katika jangwa la Sinai. Waisraeli wakafanya yote kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.