Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 8:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Maana wazaliwa wote wa kwanza kati ya Waisraeli ni wangu, wanadamu na nyama; maana niliwatakasa kwa ajili yangu siku nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza katika inchi ya Misri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 8:17
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Aliua wazaliwa wa kwanza katika inchi yao, ndilo chipukizi la kwanza la jamaa za Wamisri.


Aliwaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, wazaliwa wa watu na wa nyama vilevile.


Aliwaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri; ndilo chipukizi la kwanza katika kambi la Hamu.


Katikati ya usiku, Yawe akawaua wazaliwa wa kwanza wote wa Misri. Wote walikufa, tangu muzaliwa wa kwanza wa mufalme wa Misri, murizi wa ufalme, mpaka muzaliwa wa kwanza wa mufungwa katika kifungo. Hata wazaliwa wa kwanza wa nyama nao walikufa.


“Unitakasie wazaliwa wote wa kwanza, maana wazaliwa wote wa kwanza wa Waisraeli ni wangu, ikuwe wanaume au wanyama.”


Hema la mukutano na mazabahu nitavifanya vitakatifu. Vilevile Haruni na wana wake nitawatakasa kusudi wanitumikie kama makuhani.


Niliwapa vilevile Sabato zangu zikuwe kitambulisho kati yangu na wao, wapate kujua kwamba mimi ni Yawe ninayewatakasa.


Hairuhusiwi kumutakasa muzaliwa wa kwanza wa nyama. Kufuatana na sheria, huyo ni wa Yawe, akuwe ni ngombe au kondoo.


maana kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri nilijitakasia kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli; kila muzaliwa wa kwanza wa mwanadamu hata wa nyama; wao watakuwa wangu. Mimi ni Yawe.


Sasa ninawatwaa Walawi pahali pa wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli,


Imeandikwa katika Sheria ya Bwana: “Kila muzaliwa wa kwanza wa kiume atatolewa kwa Bwana.”


Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?


Ninajitoa kwako kabisa mimi mwenyewe kwa ajili yao, kusudi wao vilevile wapate kujitoa kwako kabisa.


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Kwa njia ya imani, alianzisha sikukuu ya Pasaka, na kuamuru damu inyunyizwe, kusudi malaika mwangamizaji asiwaue wazaliwa wa kwanza wanaume wa Waisraeli.


Kwa mapenzi yake mwenyewe alitupatia sisi uzima kwa njia ya ujumbe wa kweli, kusudi tupate kuwa kama mavuno ya kwanza katikati ya viumbe vyake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ