Kisha Yawe wa majeshi akasema hivi: Hao watakuwa watu wangu. Watakuwa urizi wangu wa kipekee siku ile nitakaposimama kufanya jambo ninalokusudia. Sitawazuru kama vile baba asivyomuzuru mwana wake anayemutumikia.
Ni mimi niliyewachagua wandugu zenu Walawi kati ya Waisraeli kama vile toleo kwenu. Wao wametengwa kwa ajili yangu mimi Yawe, kusudi wafanye kazi katika hema la mukutano.
Sasa nimechagua Walawi kati ya Waisraeli wote, pahali pa kila muzaliwa wa kwanza mwanaume anayefungua tumbo la mama yake katika kila jamaa ya Israeli. Walawi ni wangu,
Sasa, utenge Walawi wote kuwa wangu pahali pa wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli. Vilevile, utenge ngombe wa Walawi wote pahali pa wazaliwa wa kwanza wa ngombe wa Waisraeli. Mimi ni Yawe.
Maana wazaliwa wote wa kwanza kati ya Waisraeli ni wangu, wanadamu na nyama; maana niliwatakasa kwa ajili yangu siku nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza katika inchi ya Misri.
Wakati huo, Yawe akachagua watu wa kabila la Lawi wakuwe wanabeba Sanduku la Agano la Yawe, wamutumikie kama vile makuhani na kubariki watu kwa jina lake hata hivi leo.
Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.