Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 8:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kisha Walawi wataweka mikono yao juu ya vichwa vya ngombe dume hao; mumoja wao utamutoa kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, na huyo mwingine utamutoa kuwa sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwangu, kwa kuwafanyia Walawi upatanisho.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 8:12
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha utamuleta yule mwana-ngombe dume mbele ya hema la mukutano. Haruni na wana wake wataweka mikono yao juu ya kichwa cha mwana-ngombe yule


ataweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama wa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, ambayo itakubaliwa kwa ajili ya kumufanyia huyo mutu upatanisho.


Ataleta vilevile hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kadiri anavyoweza mumoja atakuwa kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.


Haruni atatoa ngombe dume wa sadaka ya zambi kwa ajili yake mwenyewe, na kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya jamaa yake, kisha atachinja ngombe dume yule wa sadaka ya zambi.


Haruni ataweka mikono yake juu ya kichwa cha huyo beberu muzima na kuungama juu yake zambi zote za watu wa Israeli, makosa yao yote na zambi zao zote; naye ataziweka zote juu ya kichwa cha yule mbuzi. Kisha atamwacha huyo beberu aende katika jangwa akipelekwa kule na mutu yeyote anayekuwa tayari.


Haruni atatoa huyo ngombe dume kwa sadaka ya kuondoa zambi kwa ajili yake mwenyewe na kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na jamaa yake.


Wazee wao wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ngombe dume, kisha atachinjwa mbele ya Yawe.


Kwa hiyo atamufanya ngombe dume huyu kama alivyomufanya yule mwingine wa sadaka kwa ajili ya zambi. Basi, huyo kuhani atawafanyia watu ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi, nao watasamehewa.


Kisha ataondoa mafuta yote kama vile anavyoondoa mafuta ya mwana-kondoo wa sadaka ya amani na kuhani atayateketeza juu ya mazabahu, pamoja na sadaka zinazotolewa kwa Yawe kwa moto. Kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.


Ataleta huyo ngombe dume muchanga kwenye mulango wa hema la mukutano, mbele ya Yawe. Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha ngombe dume huyo na kumuchinja mbele ya Yawe.


Lakini kama hawezi kutoa mwana-kondoo wa sadaka ya kosa kwa ajili ya zambi aliyotenda, basi atamuletea Yawe hua wawili au vitoto viwili vya njiwa, mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto.


Kisha Musa akaleta ngombe wa sadaka kwa ajili ya zambi, naye Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha ngombe huyo.


Musa akamuchinja huyo ngombe, akatwaa damu akapakaa pembe za mazabahu pande zote kwa kidole chake kwa kuitakasa. Kisha akatwaa damu iliyobaki akaimwanga chini kwenye tako la mazabahu ambayo alitakasa kwa kuifanyia ibada ya upatanisho.


Kisha, Musa akaleta kondoo dume wa sadaka ya kuteketezwa. Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo.


Yawe ameamuru tufanye kama vile tulivyofanya leo kusudi tuwafanyie ibada ya upatanisho.


Halafu Musa akamwambia Haruni: Kwenda kwenye mazabahu, utolee pale sadaka yako kwa ajili ya zambi na sadaka ya kuteketezwa na kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yako na kwa ajili ya watu wa Israeli. Kisha tolea pale sadaka za watu na kuwafanyia ibada ya upatanisho kama vile Yawe alivyoamuru.


na kumutolea Yawe zawadi zake: mwana-kondoo dume mumoja wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; mwana-kondoo dike mumoja wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya zambi; na kondoo dume mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya amani.


Kuhani atamutolea Yawe vitu vyote hivi pamoja na sadaka yake ya zambi na sadaka yake ya kuteketezwa.


Kisha utawasimamisha Walawi mbele ya Haruni na wana wake na kuwaweka mbele yangu kama vile sadaka ya kutikiswa.


Kisha watatwaa mwana-ngombe dume mumoja pamoja na sadaka yake ya vyakula, ni kusema unga laini uliochanganywa na mafuta; nawe utatwaa mwana-ngombe dume wingine kwa ajili ya zambi.


Na kufuatana na Sheria, karibu vitu vyote vinatakaswa kwa damu, nazo zambi haziwezi kusamehewa pasipo kumwangwa kwa damu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ