Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 7:89 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

89 Wakati Musa alipoingia ndani ya hema la mukutano kwa kuongea na Yawe, akasikia sauti kutoka upande wa juu wa kiti cha rehema, kilichokuwa juu ya Sanduku la Agano, kutoka kati ya wale makerubi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 7:89
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alitengeneza kwa mbao za mizeituni sanamu za makerubi wawili, kila sanamu ikiwa na metre ine na nusu kwenda juu, akaziweka katika chumba cha ndani kabisa.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo. Zaburi ya Asafu.


Yawe anatawala, mataifa yanatetemeka! Ameikaa juu ya makerubi, nayo dunia inatikisika!


Kisha, lile wingu likafunika lile hema la mukutano na utukufu wa Yawe ukajaza hema.


Musa akashindwa kuingia ndani ya hema la mukutano kwa sababu hilo wingu lilikaa juu yake na utukufu wa Yawe ukajaa mule.


Yawe akamwita Musa na kuongea naye katika hema la mukutano, akamwambia:


Katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, mwaka wa pili nyuma ya watu wa Israeli kutoka Misri, Yawe akasema na Musa ndani ya hema la mukutano katika jangwa la Sinai, akamwambia hivi:


Nitashuka kule na kuzungumuza nawe; nitatwaa sehemu ya roho niliyokupa, niwape watu hao. Nao watabeba muzigo wa kuwatunza watu hawa pamoja nawe, kusudi usibebe muzigo huo peke yako.


Mimi ninaongea naye kinywa kwa kinywa, waziwazi na si kwa kutumia mafumbo. Yeye ameliona umbo langu mimi Yawe. Kwa nini, basi, hamukuogopa kusema vibaya juu ya mutumishi wangu Musa?


Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


Mungu aliwafunulia wale manabii kwamba ujumbe ule walioutangaza haukuwaelekea wao wenyewe, lakini uliwaelekea ninyi. Na sasa ujumbe ule umetangazwa kwenu na wale waliowahubiri Habari Njema kwa uwezo wa Roho Mutakatifu aliyetumwa toka mbinguni. Hata wamalaika vilevile wanatamani kujua mambo hayo.


Kwa hiyo, walituma watumishi kule Shilo, nao wakalileta Sanduku la Agano la Yawe wa majeshi ambaye anatawala juu ya makerubi. Wale wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi walikuja pamoja na lile Sanduku la Agano la Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ