Basi, mufalme Solomono akawakusanya mbele yake kule Yerusalema wazee na viongozi wote wa makabila na wa ukoo za Waisraeli kusudi waliondoe Sanduku la Agano la Yawe katika muji wa Daudi, ni kusema Sayuni.
Nao wakubwa wake, kwa mapenzi yao, waliwapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zakaria na Yehieli, wasimamizi wa nyumba ya Mungu, waliwapa makuhani wana-kondoo na wana-mbuzi elfu mbili mia sita na ngombe dume mia tatu kwa ajili ya sadaka za Pasaka.