Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 7:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Yawe akamwambia Musa: Kila siku kiongozi mumoja atatoa sadaka yake kwa ajili ya kutakasa mazabahu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 7:11
5 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Viongozi hao wakatoa sadaka kwa ajili ya kuitakasa mazabahu siku ile ilipopakwa mafuta; walitoa sadaka zao mbele ya mazabahu.


Wale waliotoa sadaka ni hawa: Siku ya kwanza: Nasoni mwana wa Aminadabu, wa kabila la Yuda; Siku ya pili: Netaneli mwana wa Suari, wa kabila la Isakari; Siku ya tatu: Eliabu mwana wa Heloni, wa kabila la Zebuluni; Siku ya ine: Elisuri mwana wa Sedeuri, wa kabila la Rubeni: Siku ya tano: Selumieli mwana wa Suri-Shadai, wa kabila la Simeoni; Siku ya sita: Eliasafu mwana wa Deueli, wa kabila la Gadi; Siku ya saba: Elisama mwana wa Amihudi, wa kabila la Efuraimu; Siku ya nane: Gamalieli mwana wa Pedasuri, wa kabila la Manase; Siku ya tisa: Abidani mwana wa Gideoni, wa kabila la Benjamina; Siku ya kumi: Ahiezeri mwana wa Amishadai, wa kabila la Dani; Siku ya kumi na moja: Pagieli mwana wa Okrani, wa kabila la Aseri; Siku ya kumi na mbili: Ahira mwana wa Enani, wa kabila la Nafutali. Hii ni sadaka iliyotolewa na kila mumoja: sahani moja ya feza yenye uzito wa kilo moja na nusu na beseni moja la feza lenye uzito wa grama mia nane kulingana na vipimo vya hema takatifu; sahani na beseni hilo vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula; kisahani kimoja cha zahabu chenye uzito wa grama mia moja na kumi kikiwa kimejazwa ubani; mwana-ngombe dume mumoja, kondoo dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja wa mwaka mumoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; beberu mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi; ngombe dume wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mumoja kwa ajili ya sadaka za amani.


kwa maana Mungu hataki sisi tuishi katika fujo, lakini katika amani. Sawa vile inavyokuwa desturi katika makanisa yote ya watu wa Mungu,


Lakini maneno yote yatendeke katika usawa na katika utaratibu.


Ijapokuwa mimi ni mbali nanyi kwa mwili, lakini mimi ni pamoja nanyi kwa roho, nami ninafurahi kuona namna munavyoishi katika utaratibu muzuri na kusimama imara katika imani mbele ya Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ