Naye Solomono alimutolea Yawe sadaka za amani: ngombe elfu makumi mbili na mbili na kondoo elfu mia moja na makumi mbili. Hivi ndivyo mufalme na watu wote wa Israeli walivyozindua nyumba ya Yawe.
Naye Solomono akamutolea ngombe elfu makumi mbili na mbili na kondoo elfu mia moja makumi mbili. Hivi ndivyo Solomono na watu wote walivyozinduwa nyumba ya Mungu.
Siku ya nane, walikusanyika wakafanya sikukuu nyuma ya muda wa siku saba, walizotumia kwa kutakasa meza ya matoleo ya sadaka, na siku saba nyingine za sikukuu.
Kisha wakati wa kuzindua ukuta wa Yerusalema Walawi wakatafutwa kila pahali walipokaa kwa kuja Yerusalema kusherehekea kwa furaha pamoja na shukrani na nyimbo, wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
Siku hiyo, watu wakatoa sadaka nyingi na kufurahi maana Mungu aliwafanya kuwa na furaha kubwa. Vilevile wanawake na watoto, wote wakafurahi. Vigelegele vya furaha toka katika Yerusalema vikasikilika mbali.
Siku Musa alipomaliza kusimamisha hema takatifu, akalimiminia mafuta na kulitakasa pamoja na vyombo vyake vyote. Akamiminia mazabahu mafuta na kuitakasa pamoja na vyombo vyake vyote.
Jumla ya matoleo ya sadaka za viongozi wa Israeli kwa ajili ya mazabahu siku ilipotakaswa ilikuwa: sahani za feza kumi na mbili, beseni za feza kumi na mbili, na visahani vya zahabu kumi na viwili.
na kwa ajili ya sadaka ya amani, jumla ya nyama waliotolewa ilikuwa ngombe dume makumi mbili na wane, kondoo dume makumi sita, beberu makumi sita, na wana-kondoo dume wa mwaka mumoja makumi sita. Hiyo ndiyo iliyokuwa sadaka iliyotolewa kwa ajili ya mazabahu, kisha mazabahu hayo kupakwa mafuta.
“Kisha wakubwa watawaambia watu: ‘Kuna mutu yeyote hapa aliyejenga nyumba mupya lakini hajaizindua? Arudie kwake, kusudi asikufie kwenye vita na mutu mwingine aizindue.