Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 6:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Yawe awaonyeshe wema wake na kuwapa amani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 6:26
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe awape watu wake nguvu! Yawe awabariki watu wake kwa amani!


Muangalie mutu mukamilifu, mutu wa usawa; mutu anayependa amani anajaliwa wazao.


Mutoe sadaka zinazokuwa sawa, na kumutumainia Yawe.


Katika huzuni yangu, ninakumbuka jinsi nilivyokwenda na kundi la watu na kuwaongoza kwenda katika nyumba ya Mungu wakipiga vigelegele vya shukrani, kundi la watu likifanya sherehe!


Kwa mukono wako mwenyewe uliyafukuza mataifa, na mahali pao ukawaikalisha watu wako; uliyaazibu mataifa, na kuwafanikisha watu wako.


Haki na sheria ndio musingi wa utawala wako; wema na uaminifu vinakutangulia!


Wewe, ee Yawe, umetupatia amani; umefanikisha shuguli zetu zote.


Ee Mungu, unawaweka katika amani wanaokuwa imara, unawaweka katika amani kwa sababu wanakutegemea.


Mimi nitawapa amani, amani kwa wanaokuwa mbali na wanaokuwa karibu! –Ni Yawe anayesema hivyo.– Mimi nitawaponyesha.


Kwa silaha zao wataitawala inchi ya Asuria, na kuirizi inchi ya Nimurodi. Watatuokoa toka katika mikono ya Waasuria, watakapoingia katika inchi yetu na kuanza kuishambulia.


“Sifa kwa Mungu juu mbinguni, na amani katika dunia kwa watu anaowapenda.”


“Ninawaachia amani; ninawapa amani yangu. Siwapatii ninyi amani hii kama dunia inavyoitoa. Musifazaike wala musiogope.


Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”


Yesu akawaambia tena: “Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma, mimi ninawatuma ninyi vilevile.”


Ilipotimia juma moja nyuma ya pale, wanafunzi wa Yesu wakakusanyika tena ndani ya nyumba ile ile, na mara hii Toma alikuwa pamoja nao. Ijapokuwa milango ilikuwa imefungwa, Yesu akawatokea tena, akasimama katikati yao na kusema: “Amani kwenu!”


Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.


Umenionyesha njia za uzima, utanijaza furaha nitakapokuwa karibu nawe.’


Basi, Mungu anayekuwa musingi wa matumaini, awajaze furaha kamili na amani kutokana na imani yenu; hata tumaini lenu lipate kuongezeka kwa nguvu ya Roho Mutakatifu.


Basi Mungu anayeleta amani akuwe pamoja nanyi wote. Amina!


Sasa kufuatana na vile tumekwisha kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani, kunakuwa sasa amani kati yetu na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.


Ninawatakia wandugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Bwana Yesu Kristo.


Na amani ya Mungu inayopita ufahamu wa mutu yeyote, italinda mioyo yenu na nia zenu salama katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Bwana wa amani mwenyewe awape amani siku zote na kwa njia zote. Bwana akuwe pamoja nanyi wote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ