Yosefu alipoinua macho yake na kumwona Benjamina, ndugu yake, mutoto wa mama yake, akasema: “Huyu ndiye ndugu yenu mudogo muliyeniambia habari zake? Mungu akubariki, mwana wangu!”
Kwa hiyo, ee Mungu, usikilize malalamiko yangu na maombi yangu mimi mutumishi wako. Kwa ajili ya heshima yako, ulionee tena hekalu lako lililoharibika huruma.
Kwa hiyo sasa enyi makuhani, mumwombe Mungu kusudi atuhurumie. Yawe wa majeshi anasema hivi: Ikiwa munamutolea matoleo ya aina hiyo, kweli atawakubali?
Ninawaandikia ninyi wote wapenzi wa Mungu munaokaa Roma, mulioitwa kuwa watu wake watakatifu. Ninawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.