Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 6:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Yawe awabariki na kuwalinda;

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 6:24
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mimi niko pamoja nawe, nitakulinda popote utakapoenda na kukurudisha katika inchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapotimiza ahadi niliyokupa.”


Kwa hiyo, ninakuomba nyumba yangu mimi mutumishi wako ipate kudumu milele mbele yako. Wewe umesema. Kwa baraka zako nyumba yangu itabarikiwa milele.”


Yawe akubariki kutoka Sayuni; yeye aliyeumba mbingu na dunia.


Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche chini ya kivuli cha mabawa yako,


Ee Mungu, uwaokoe watu wako; uwabariki watu hao wanaokuwa mali yako. Ukuwe muchungaji wao na kuwalinda milele.


Maana Mungu atawaamuru wamalaika wake, wakulinde popote unapoenda.


Mimi, Yawe, ni mulimaji wake; ninalimwangilia maji kila wakati. Ninalilinda usiku na muchana, kusudi lisiharibiwe na mutu yeyote.


Mimi Yawe nimekuita kutenda haki, nimekushika mukono na kukulinda. Kwa njia yako nitafanya ahadi na watu wote, wewe utakuwa mwangaza wa mataifa.


Kwa hiyo, ee Mungu, usikilize malalamiko yangu na maombi yangu mimi mutumishi wako. Kwa ajili ya heshima yako, ulionee tena hekalu lako lililoharibika huruma.


Mimi sitabaki tena katika dunia, lakini wao wangali katika dunia na mimi ninakuja kwako. Baba Mutakatifu, uwalinde kwa uwezo wa jina lako, lile jina ulilonipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja.


Kwa maana kama ukimwomba Mungu ndani ya roho tu kwa kumushukuru, mutu asiyeelewa kitu anayehuzuria katika mukutano hawezi kusema amina kwa kuitikia maombi yako ya kushukuru. Ni kwa sababu hasikii mambo unayosema.


Ninawatakia neema wale wote wanaomupenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usiokuwa na mwisho.


Ninawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.


Na amani ya Mungu inayopita ufahamu wa mutu yeyote, italinda mioyo yenu na nia zenu salama katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa, alinde uzima wenu wote ndiyo roho, moyo na mwili wenu, kusudi visikutiwe na kosa wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudia.


Ninyi ambao kwa imani munalindwa salama kwa nguvu za Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa kwa mwisho wa nyakati.


Basi yeye anayeweza kuwalinda kusudi musianguke, na kuwasimamisha ninyi mbele ya utukufu wake pasipo kilema na kwa furaha kubwa,


Nyuma ya muda, Boazi akafika kutoka Betelehemu, akawasalimia wavunaji, akasema: “Yawe akuwe nanyi.” Nao wakamujibu: “Yawe akubariki.”


Anayalinda maisha ya waaminifu wake, lakini anaangamiza maisha ya waovu katika giza. Maana, mwanadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ