basi wote wawili watakwenda kwa kuhani na kupeleka sadaka inayotakiwa, ni kusema sehemu ya kumi ya unga wa shayiri; lakini bila kuitia mafuta au ubani, kwa sababu ni sadaka ya vyakula ya mume anayekuwa na wivu kwa muke wake, kwa ukumbusho wa kosa.
Kuhani atamuweka mbele ya Yawe na kumufunua nywele na kumupa sadaka hiyo ya vyakula inayotolewa kwa sababu ya wivu wa mume wake. Kuhani mwenyewe atashikilia kile chombo chenye maji machungu yanayoleta laana.