Kulikuwa watu wane wenye ugonjwa wa ukoma waliokuwa inje ya milango ya muji wa Samaria ambao walisemezana, wao kwa wao: “Mbona tunakaa hapa tukikufa na njaa?
Mwenye ukoma yeyote atavaa nguo zilizochanika, nywele zake hatazichanuliwa, na mudomo wake wa juu ataufunika na atalalamika akisema: Mimi ni muchafu, mimi ni muchafu.
Huyo mutu atafua nguo zake, atanyoa nywele zake, na kuoga, naye atakuwa safi. Nyuma ya hayo atarudi ndani ya kambi, lakini atakaa inje ya hema lake kwa muda wa siku saba.
Wingu lilipoondoka juu ya hema la mukutano, Miriamu akaonekana yuko na ukoma, mweupe kama teluji. Haruni alipogeuka na kumwangalia Miriamu, akashangaa kuona kwamba ameshikwa na ukoma.
Lakini Yawe akamwambia Musa: Kama baba yake angemutemea mate kwenye uso, basi, hangepata haya kwa siku saba? Basi, umutoe inje ya kambi akae kule muda wa siku saba, kisha unaweza kumuruhusu arudi katika kambi.
Wote wale wanaokuwa kati yenu ambao wameua mutu au kugusa maiti wanapaswa kukaa inje ya kambi kwa muda wa siku saba; mujitakase pamoja na mateka wenu katika siku ya tatu na ya saba.