Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 4:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Wakati wa kuvunja kambi, Haruni na wana wake wataingia katika hema, na kushusha pazia linalokuwa mbele ya Sanduku la Agano, kisha walifunike kwa pazia hilo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 4:5
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walawi wakalibeba juu ya mabega yao wakitumia miti yake ya kuibebea kama Musa alivyoamuru, kulingana na neno la Yawe.


Kwa hiyo, Walawi hawatahitaji tena kubeba hema takatifu au vyombo vyake vya ibada.”


Akatengeneza pazia kwa kitambaa cha kitani safi, cha rangi ya samawi, ya rangi nyekundu-nyeusi na nyekundu. Akalichora kwa michoro ya makerubi.


Alitengeneza pazia la nyuzi za rangi ya samawi, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa. Pazia hilo lilipambwa na makerubi kwa ufundi.


Ndani ya hema hilo utaweka lile Sanduku la Agano, kisha weka pazia mbele yake.


Mazabahu ya zahabu ya kufukizia ubani utaiweka mbele ya Sanduku la Agano, kisha utatundika pazia kwenye mulango wa hema takatifu.


Katika mulima huuhuu, Yawe ataliondoa wingu la huzuni lililowafunika watu wote, kifuniko cha uchungu juu ya mataifa yote.


Akamwambia: Umwambie ndugu yako Haruni asiingie katika Pahali Patakatifu nyuma ya pazia wakati usiokubaliwa. Asiingie pahali pale maana ndipo nitakapotokea katika wingu juu ya kiti cha rehema. Asipotii, atakufa.


Wale waliokuwa chini ya bendera ya jeshi la kabila la Yuda, wakatangulia, kundi moja kisha lingine. Kiongozi wao alikuwa Nasoni mwana wa Aminadabu.


Kisha Haruni na wana wake kufunika Pahali Patakatifu pamoja na vyombo na vifaa vyake vyote, wakiwa tayari kuanza safari, watu wa ukoo wa Kohati watakuja na kuvibeba. Lakini wao, hawaruhusiwi kabisa kugusa vyombo hivyo vitakatifu, kusudi wasikufe. Hiyo ndiyo kazi ya ukoo wa Kohati kila wakati hema la mukutano linapohamishwa.


Hii ndiyo itakayokuwa kazi ya wana wa Kohati, kuelekea vitu vitakatifu kabisa.


Lakini Musa hakuwapa Wakohati kitu chochote kwa sababu wao walikuwa na utumishi wa kutunza vitu vitakatifu ambavyo vilipaswa kubebwa juu ya mabega.


Na saa ile ile pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini. Inchi ikatetemeka, mawe makubwa yakapasuka,


Basi, Musa akaandika sheria hiyo, akawapa makuhani wa ukoo wa Lawi ambao walikuwa wakibeba Sanduku la Agano la Yawe, na wazee wote wa Israeli.


Yeye ametufungulia njia mupya ya uzima, inayopitia katika pazia, maana yake mwili wake mwenyewe.


Na nyuma ya pazia lililotenga kile chumba cha kwanza, kulikuwa chumba kingine kilichoitwa Pahali Patakatifu Sana.


Yawe aliwaua wakaaji makumi saba wa muji wa Beti-Semesi, kwa sababu waliangalia ndani ya Sanduku lake. Watu waliomboleza kwa sababu Yawe alikuwa amefanya mauaji makubwa kati yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ