37 Hii ndiyo hesabu ya watu wa jamaa ya Wakohati, ambao walitumika katika hema la mukutano, ambao Musa na Haruni wakawahesabu kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
Hayo ndiyo masharti, maagizo na sheria ambazo Yawe aliwapa watu wa Israeli kule kwenye mulima Sinai kwa njia ya Musa.
Basi, Musa akawahesabu kufuatana na neno la Yawe, kama vile alivyomwamuru.
Jamaa za Waamuramu, Waisari, Wahebroni na Wauzieli zilitokana na Kohati; hizi ndizo zilizokuwa jamaa za Wakohati.
Hesabu yao kufuatana na jamaa zao ilikuwa watu elfu mbili mia saba na makumi tano.
Hesabu ya watu wa ukoo wa Gersoni kufuatana na jamaa zao,
wenye umri kati ya miaka makumi tatu na makumi tano, na ambao walifaa kwa kazi na ubebaji katika hema la mukutano,
Kila mumoja alipewa kazi yake ya kufanya juu ya kubeba hema la mukutano, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.