Wake wako wote na watoto wako watapelekwa kwa Wakaldea, nawe mwenyewe hautaponyoka. Utakamatwa mateka na mufalme wa Babeli na muji huu utateketezwa kwa moto.
Basi, kwa kuwaepusha wasipate kuuawa kwa kukaribia vyombo hivyo vitakatifu sana utafanya hivi: Haruni na wana wake wataingia na kumupangia kila mumoja wao mapaswa yake na kazi yake.
Yawe aliwaua wakaaji makumi saba wa muji wa Beti-Semesi, kwa sababu waliangalia ndani ya Sanduku lake. Watu waliomboleza kwa sababu Yawe alikuwa amefanya mauaji makubwa kati yao.