Kwa kutumia sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu walifuma nguo za kuvaa wakati wa kutumika katika Pahali Patakatifu. Walimushonea Haruni nguo takatifu kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
na nguo zote zilizofumwa vizuri kabisa kwa ajili ya kazi ya Pahali Patakatifu, ni kusema nguo takatifu za kuhani Haruni, na za wana wake kwa ajili ya kazi za ukuhani.
Juu yake wataweka vyombo vyote vinavyotumika katika ibada kwenye mazabahu: vyetezo, makanya, miiko na mabakuli. Kisha, juu yake watatandaza kifuniko cha ngozi laini ya mbuzi na kuiingiza miti yake ya kulibebea.