Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Watatwaa vyombo vyote vinavyotumika katika Pahali Patakatifu, watavifunga kwa kitambaa cha rangi ya samawi na kuvifunika kwa ngozi laini ya mbuzi, kisha wataviweka juu ya miti yake ya kubebea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 4:12
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walawi wengine walisimamia vyombo vilivyotumika wakati wa ibada. Walihitajika kuvihesabu wakati vilipotolewa na wakati viliporudishwa.


Wengine walichaguliwa kusimamia vifaa vya hekalu, na vyombo vyote vitakatifu, na unga safi, divai, mafuta ya mizeituni, ubani na marasi.


Hiramu akatengeneza vyungu, vipao na mabeseni. Basi Hiramu akamaliza kazi aliyomufanyia mufalme Solomono juu ya nyumba ya Mungu;


Halafu vyungu, vipao na kanya na vyombo vingine vyote vya nyumba ya Yawe ambavyo Huruma-Abi alimutengenezea mufalme Solomono, vilikuwa vya shaba iliyoangarishwa.


Solomono alitengeneza vitu vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Mungu: mazabahu ya zahabu na meza za mikate mitakatifu;


makasi na mabeseni, sahani za kuwekea ubani na vyetezo vya kubebea moto, vyote vya zahabu safi, pete za hekalu za milango ya Pahali Patakatifu Sana, na za milango mingine ya vyumba vya ndani, zote zilitengenezwa na zahabu.


ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, ngozi za mbuzi, mbao za mujohoro,


Utatengeneza hema hiyo na vifaa vyake kulingana na mufano nitakaokuonyesha.


nguo takatifu ya kuhani Haruni na wana wake ambao watafanya kazi ya ukuhani,


Watatunza vyombo vyote vya hema la mukutano na kuwasaidia Waisraeli wanapofanya kazi zao kwenye hema takatifu.


Halafu watatandaza kitambaa cha rangi ya samawi juu ya mazabahu ya zahabu na kuifunika kwa ngozi laini ya mbuzi. Halafu wataingiza miti yake ya kuibebea.


Wataondoa majivu juu ya mazabahu na juu yake watatandaza kitambaa cha rangi ya zambarau.


Juu yake wataweka kifuniko cha ngozi laini ya mbuzi, kisha watatandaza juu yake kitambaa cha rangi ya samawi tupu. Halafu wataingiza miti ya kulibebea sanduku hilo.


Juu ya meza ya kutolea mikate inayowekwa mbele ya Yawe watatandaza kitambaa cha rangi ya samawi na juu yake wataweka sahani, visahani vya ubani, bakuli na bilauri, kwa ajili ya kutolea sadaka za kinywaji. Siku zote kutakuwa mukate juu ya meza.


Watatwaa kitambaa cha rangi ya samawi ambacho watafunikia kinara cha taa na taa zake, makasi zake, sinia zake na vyombo vyote vinavyotumiwa kukiwekea mafuta.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ