Hivyo mupaka utakwenda kutokea bahari ya Mediteranea kuelekea mashariki mpaka katika muji wa Hazorenoni ukipakana na maeneo ya Damasiki na Hamati kwa upande wa kaskazini.
Haya ndiyo majina ya makabila na sehemu zao: Kuanzia kwenye mupaka wa kaskazini kwenye barabara ya Hetiloni mpaka kuingia Hamati hata Hazorenoni unaokuwa katika Damasiki na Hamati upande wa kaskazini na kuendelea kutoka mashariki mpaka magaribi. Eneo hilo litakuwa la kabila la Dani.