Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 32:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mbona munawavunja moyo Waisraeli wasiende katika inchi ambayo Yawe amewapa?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 32:7
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakamwambia Musa: Tuliifikia inchi uliyotutuma tuipeleleze; hiyo ni inchi inayotiririka maziwa na asali, na hili ni tunda lake.


Lakini watu walioandamana naye kupeleleza inchi wakasema: Hatutaweza kupigana na watu hao; wao wana nguvu kuliko sisi.


Haya ndiyo majina ya watu hao kulingana na makabila yao: Kabila la Rubeni: Samua mwana wa Zakuri. Kabila la Simeoni: Safati mwana wa Hori. Kabila la Yuda: Kalebu mwana wa Yefune. Kabila la Isakari: Igali mwana wa Yosefu. Kabila la Efuraimu: Hosea mwana wa Nuni. Kabila la Benjamina: Palti mwana wa Rafu. Kabila la Zebuluni: Gadieli mwana wa Sodi. Kabila la Yosefu (ni kusema kabila la Manase): Gadi mwana wa Susi. Kabila la Dani: Amieli mwana wa Gemali. Kabila la Aseri: Seturi mwana wa Mikaeli. Kabila la Nafutali: Nabi mwana wa Wofusi. Kabila la Gadi: Geueli mwana wa Maki.


Waisraeli wakafunga safari kutoka mulima Hori, wakapitia njia inayoelekea bahari Nyekundu kusudi wazunguke inchi ya Edomu. Lakini katika njia watu wakavunjika moyo.


Musa akawajibu watu wa makabila ya Gadi na Rubeni: Munataka kubaki hapa wakati wandugu zenu Waisraeli wanakwenda kwa vita?


Wao walikwenda mpaka bonde la Eskoli, wakaiona inchi, lakini waliporudi, wakavunja Waisraeli moyo kusudi wasiingie katika inchi Yawe aliyowapa.


Lakini Paulo akajibu: “Kwa sababu gani munalia na kunivunja moyo? Mimi niko tayari, si kwa kufungwa tu kule Yerusalema, lakini hata kufa vilevile kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”


Kwa nini tuende huko wakati tumevunjika moyo kwa hofu? Wametuambia kwamba watu wa huko ni wakubwa na warefu kuliko sisi, na kwamba miji yao ni mikubwa na yenye kuta zinazofika katika mawingu. Tena wamesema kwamba waliwaona wale wazao wa Anaki!’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ