Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 32:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Basi, kama tumepata kukubaliwa mbele yako, wewe Musa, tunakuomba utupatie inchi hii ikuwe mali yetu; usituvukishe ngambo ya muto Yordani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 32:5
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ni kweli kwamba mimi mutumishi wako nimepata kukubaliwa mbele yako, nawe umenitendea mema sana kwa kuokoa maisha yangu. Lakini kwenye milima ni mbali sana. Maangamizi haya yatanikuta mbele sijafika kule, nami nitakufa.


Yoabu alianguka uso mpaka chini, na kumutakia mufalme baraka, akasema: “Leo, mimi mutumishi wako, bwana wangu mufalme, ninajua kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako, kwa kulikubali shauri langu.”


Mufalme alipomwona malkia Esteri akisimama katika kiwanja, Esteri akapata kukubaliwa mbele yake, naye akamunyooshea fimbo ya zahabu aliyokuwa akishika katika mukono wake. Esteri akakaribia, akagusa incha ya fimbo.


Yawe anasema hivi: Watu walioponyoka kuuawa, nilionyesha neema yangu kwao katika jangwa. Wakati Israeli alipotafuta kwenda kupumzika,


inchi ambayo Yawe alishinda kwa ajili ya Waisraeli, ni inchi nzuri kwa mifugo, nasi tuko na mifugo mingi sana.


Musa akawajibu watu wa makabila ya Gadi na Rubeni: Munataka kubaki hapa wakati wandugu zenu Waisraeli wanakwenda kwa vita?


Yawe akanikasirikia mimi vilevile kwa sababu yenu, akasema: ‘Hata wewe Musa hautaingia katika inchi hiyo.


Yoshua akasema: “Ole wetu, ee Bwana wetu Yawe! Kwa nini umetuvukisha muto Yordani kwa kututia katika mikono ya Waamori kusudi watuangamize? Tungalifurahi kubaki ngambo ya muto Yordani!


Hapo Ruta akamwinamia Boazi uso mpaka chini kwa unyenyekevu, akamwambia: “Nimepata namna gani kukubaliwa mbele yako? Mbona unanishugulikia ijapokuwa mimi ni mugeni tu?”


Daudi akaapa vilevile: “Hakika baba yako anajua vizuri kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako. Anafikiri kukuficha juu ya jambo hili kusudi usihuzunike atakapolitenda. Lakini kweli, kama Yawe anavyoishi na kama wewe mwenyewe unavyoishi, kati yangu na lufu kuna hatua moja tu!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ