Yairi, mutu wa kabila la Manase, alitwaa eneo lote la inchi ya Argobu, ni kusema Basani, mpaka kwenye mupaka wa Gesuri na Maka. Vijiji vyote alivipa jina lake, na mpaka leo vinajulikana kama vile ‘Vijiji vya Yairi’.
Yairi alikuwa na watoto wa kiume makumi tatu ambao walipanda juu ya punda makumi tatu na walikuwa na miji makumi tatu katika inchi ya Gileadi, ambayo mpaka leo inaitwa Miji ya Yairi.