Hesabu 32:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
32 Chini ya uongozi wa Yawe, tutavuka na silaha zetu mpaka katika inchi ya Kanana, lakini inchi tuliyopewa hapa upande wa mashariki wa Yordani itakuwa mali yetu.
Mutakapoingia katika inchi ya Kanana ambayo ninawapa kuwa urizi wenu, nami nikifanya namna ya ukoma uote katika ukuta wa nyumba fulani katika inchi mutakayorizi,
Basi, Musa akawapa watu wa makabila ya Gadi na Rubeni na nusu ya kabila la Manase mwana wa Yosefu, inchi yote ya mufalme Sihoni wa Waamori na inchi ya mufalme Ogi wa Basani pamoja na miji na maeneo yaliyokuwa kandokando ya miji hiyo.
Kitabu hiki kina maneno ambayo Musa aliwaambia watu wote wa Israeli wakati walipokuwa katika jangwa upande wa mashariki wa muto Yordani. Walikuwa katika bonde la Yordani karibu na Sufu, kati ya muji wa Parani upande mumoja na miji ya Tofeli, Labani, Hazeroti na Dizahabu upande mwingine.
“Tulipoitwaa inchi hiyo, nikawapa makabila ya Rubeni na Gadi eneo la kuanzia upande wa kaskazini wa Aroeri karibu na Arnoni na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
Hawa ndio wafalme ambao Waisraeli waliwashinda na kunyanganya inchi yao yote iliyokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani kutokea bonde la muto Arnoni mpaka kwenye mulima Hermoni na inchi yote ya Araba upande wa mashariki:
Musa mutumishi wa Yawe pamoja na Waisraeli aliwashinda wafalme hao, akawapatia inchi hizo makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase zikuwe mali yao kabisa.