Ukawapatia ushindi juu ya falme na mataifa, ukawafanyia mengi kila upande. Wakashinda inchi ya Hesiboni iliyotawaliwa na mufalme Sihoni; na tena wakashinda inchi ya Basani iliyotawaliwa na mufalme Ogi.
Juu ya inchi ya Moabu, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ole kwa watu wa Nebo, maana muji wao umeharibiwa! Kiriataimu umepatishwa haya, umetekwa, ukuta wake umebomolewa;
utukufu wa inchi ya Moabu umetoweka. Mupango ulifanywa huko Hesiboni juu yake: Basi! Tuwaangamize wasikuwe tena taifa! Nawe muji wa Madimeni utanyamazishwa, upanga utakufuatilia.
Ninakulilia wewe muzabibu wa Sibuma kuliko hata watu wa Yazeri. Matawi yako yametanda mpaka ngambo ya bahari ya Chumvi, yakafika hata mpaka Yazeri. Lakini mwangamizaji ameyarukia matunda yako ya wakati wa jua na mizabibu yako.
Kilio cha watu wa Hesiboni kinasikilika huko Eleale mpaka Yasa; kinaenea kutoka Soari mpaka Horonaimu na kufika hata Eglati-Selisia. Hata maji ya kijito Nimurimu yamekauka.
Wakimbizi wanaochoka wanasimama chini ya kivuli cha Hesiboni. Moto umewaka huko katika muji; ulimi wa moto toka nyumba ya kifalme ya Sihoni; umeteketeza mipaka ya Moabu, umeunguza milima ya hao wanaopiga kelele.
Wakati wote Waisraeli walipoishi katika muji wa Hesiboni na vijiji vyake, na muji wa Aroeri na vijiji vyake pamoja na miji yote inayokuwa kwa ukingo wa muto Arnoni kwa muda wa miaka mia tatu, kwa nini haukulikomboa eneo hilo wakati huo?